Habari za Punde

Masauni aongoza Wajumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani kutoa elimu ya Usalama Barabarani Zanzibar

 Naibu  Waziri  wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), akimuelekeza dereva bodaboda jinsi ya kufunga kofia ngumu wakati wa utoaji wa elimu kwa madereva na watumiaji wa barabara, lengo la elimu hiyo ni kuwaepusha na ajali zinazoweza kuzuilika,zoezi hilo limefanyika Visiwani Zanzibar.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni(katikati), akizungumza na dereva wa daladala  wakati wa utoaji wa elimu kwa madereva na watumiaji wa barabara, lengo la elimu hiyo ni kuwaepusha na ajali zinazoweza kuzuilika,zoezi hilo limefanyika Visiwani Zanzibar.Kushoto ni Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano,Elias Kwandikwa.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
 Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Zanzibar,Kamishna Msaidizi Robert Patrick, akiwaonyesha wajumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani sehemu ambako hutumika kwa wavuka kwa miguu ikiwa imefutika alama za pundamilia,wakati wajumbe hao walipokwenda kutoa elimu kwa madereva na abiria juu ya usalama barabarani,watatu kulia ni  Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni aliyeongoza ujumbe huo,zoezi hilo limefanyika Visiwani Zanzibar.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
 Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Nchini,Kamishna Mwandamizi Msaidizi,Fortunatus Musilimu akiwaeleza wajumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ripoti ya ajali za barabarani nchini muda mfupi kabla ya kuanza ziara ya kutembelea vituo vya daladala kutoa elimu ya kujiepusha na ajali za barabarani,wapili kulia ni  Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni aliyeongoza ujumbe huo,zoezi hilo limefanyika Visiwani Zanzibar.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni (wapili kulia), akiwaongoza wajumbe wa baraza hilo kuelekea katika vituo vya daladala kutoa elimu kwa watumiaji  wa vyombo vya moto,lengo la elimu hiyo ni kuwaepusha na ajali zinazoweza kuzuilika,zoezi hilo limefanyika Visiwani Zanzibar.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), akimsikiliza mwananchi wa  Zanzibar  wakati wa utoaji wa elimu kwa madereva na watumiaji wa barabara, lengo la elimu hiyo ni kuwaepusha na ajali zinazoweza kuzuilika, zoezi hilo limefanyika Visiwani Zanzibar.Watatu kulia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.