Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Kazi,Uwesheji,Wazee,Wanawake na Watoto katika mkutano wa utekelezaji wa malengo ya mpango kazi kwa kipindi cha Julai 2018-Juni 2019 na mpango kazi wa mwaka 2019-2020 katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo,[Picha na Ikulu.] 23/08/2019.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ameeleza haja kwa uongozi wa Wizara ya Kazi, Uwezeshajai Wazee, Wanawake na Watoto kuandaa utaratibu maalum wa kuangalia afya za wafanyakazi kabla na baada ya kuajiriwa kazini.
Hayo aliyasema leo, Ikulu mjini Zanzibar
alipokutana na uongozi wa Wizara ya Kazi, Uwezeshajai Wazee, Wanawake na Watoto
wakati ilipowasilisha utekelezaji wa Mpango Kazi wa Julai 2018 hadi Juni 2019 sambamba na Mpango Kazi wa
Utekelezaji kwa mwaka 2019/2020.
Alieleza kuwa utaratibu huo utaweza kurahisisha na
kutambua afya za wafanyakazi kwani tayari Serikali inao utaratibu mzuri wa
kuwashughulikia wafanyakazi wakati wanapopata ajali wakiwa kazini lakini
haipendezi kuona afya za wafanyakazi hazitambuliwi wakati wapo kazi.
Hivyo, Rais
Dk. Shein alisisitiza haja kwa Wizara hiyo kukaa pamoja na kushirikiana na Wizara
ya Afya katika kuandaa uataratibu huo maalum utakaowasaidia wafanyakazi
kutambua afya zao wakati wote wakaiwa kazini.
Aidha, Rais Dk. Shein ameiagiza Wizara hiyo
kufikiria namna ya kuongeza mtaji wa Mfuko wa Uwezeshaji wa Wananchi Kiuchumi
ili mfuko huo uweze kukidhi mahitaji ya wananchi ambao idadi yao imekuwa
ikiongezeka siku hadi siku.
Amesema kuwa katika kipindi cha miaka minane iliyopita
Serikali imechukua juhudi kubwa za kuwawezesha wananchi kupitia mfuko huo
ambapo matunda yake yamekuwa yanaonekana wazi wazi.
Pamoja na hayo, Rais Dk. Shein alieleza haja kwa
Wizara hiyo kuandaa utaratibu utakaoweza kusaidia kubainisha na kutambua hali
ya changamoto ya udhalilishaji wa wanawake na watoto ambayo imekuwa tatizo
katika jamii hivi sasa.
Ameeleza matumaini yake makubwa kwa Wizara hiyo na kusisitiza jinsi anavyofarajika na
utendaji kazi kwa uongozi na wafanya kazi wote wa Wizara hiyo na kuwasisitiza kuendeleza
umoja na mshikamano wao ili waweze kupata mafanikio zaidi.
Pamoja na hayo, Rais Dk. Shein alisisitiza haja
kwa waajiri wa sekta binafsi kufuata sheria, taratibu na kanuni za uajiri
katika kuhakikisha wanarekebisha maslahi
ya wafanyakazi wao kwani huo ni uamuzi wa Serikali.
Rais Dk. Shein alitumia fursa hiyo kuupongeza
uongozi wa Wizara hiyo kwa kuwasilisha
vyema Mpango Kazi wao huo na kupelekea mjadala huo kuwa mzuri.
Alieleza kuvutiwa kwake na tafiti nne zilizofanywa
na Wizara hiyo ukiwemo utafiti wa
kuwatambua na kuwawezesha Vijana Nguvu Kazi Zanzibar, Utafiti wa Fursa za ajira
zilizopo katika sekta ya kilimo, uvuvi na utalaii kwa vijana na utafiti wa
Pensheni Jamii.
Nae Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la
Mapinduzi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee aliipongeza kazi nzuri ya uwasilishaji
iliyofanywa na Wizara hiyo huku akisisitiza haja kwa uongozi na wafanyakazi wa
Wizara hiyo kuendeleza mashirikiano.
Mshauri wa Rais wa Zanzibar Pemba Dk. Maua Abeid
Daftari alitoa pongezi kwa uongozi wa Wizara hiyo kwa kazi nzuri wanazozifanya
huku akisisitiza haja ya kuwa na mashirikiano kati ya Wizara hiyo pamoja na
Wizara ya Katiba na Sheria.
Mapema, Naibu Waziri wa Wizara ya Kazi,
Uwezeshajai Wazee, Wanawake na Watoto Shadia Mohamed Suleiman alieleza kuwa Dira ya Wizara hiyo ni kuwa na jamii ya
Wazanzibari yenye ajira za staha, ubunifu na uwezo wa kukabiliana na umasikini
inayotokana na fursa sawa kwa watu wa makundi yote.
Naibu Waziri huyo alieleza kuwa Wizara hiyo
inaendlea na kusimmaia utekelezaji wa
Sheria na kanuni za kazi, kusimamia upatikanajiwa ajira hasa kwa bijana ndani
nan je ya nchi.
Aidha, alieleza kuwa Wizara hiyo inaendelea
kusimamia usuluhishi na uamuzi wa migogoro ya kazi sehemu za kazi, kuimarisha
usalama na afya kazini, kuongeza na kutanua program za uwezeshaji wananchi kiuchumi,
kuimarisha program za maendeleo na hifadhi ya wazee, wanawake na watoto pamoja
na kuratibu masuala la jinsia katika Sera, Sheria, Mipango na bajeti za Kitaifa
na Kisekta.
Alieleza kuwa kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019
Wizara imepata mafanikio kadhaa yakiwemo kukamilisha ujenzi wa ghorofa ya pili
ya jengo la Ofisi Kuu ya Wizara Unguja na kupata Ofisi mpya Pemba jambo ambalo
limepunguza tatizo la uhaba wa Ofisi kwa Watendji.
Pia, Wizara imefanikiwa kutoa mikopo 553 Unguja na Pemba yenye thamani ya TZS milioni
782 kwa Shehia 223 kwa Unguja na Pemba
pamoja na kufanya usajili wa
vyama vya ushirika 281.
Pamoja na hayo, Naibu Waziri huyo alieleza mafunzo
mbalimbali yaliyofanywa na Wizara hiyo pamoja na kushirikiana na Serikali ya
India, Shirika la UNDP, FAO na COSTECH kwa ajili ya wajasiriamali pamoja na
vijana wa Unguja na Pemba.
Alieleza kuwa Wizara hiyo imeendelea kuratibu,
kusimamia na kutekeleza Mpango wa pensheni Jamii kwa wazee wenye umri wa miaka
sabini na kuendelea ambapo idadi ya Wazee wanaopokea pensheni jamii imefikia
walengwa 27,990 ambapo hadi Juni, 2019 wazee wapya 2,275 wamesajiliwa na wazee
1,911 walifariki kwa mwaka 2018/2019.
Naibu Waziri huyo huyo alieleza kuwa Wizara
imeratibu upatikanaji wa ajira 2,759 Unguja na Pemba, ambapo ajira 1,555 ni za
ndani na ajira 1,204 ni za nje katika nchi za UAE na Oman, pia, Wizara imefanya
ukaguzi wa usalama na afya kazini.
Uongozi wa Wizara hiyo pia, ulimpongeza Rais Dk.
Shein kwa kuwapa maelekezo ya kutekeleza kazi zao kwa ufanisi sambamba na
anavyotekeleza ipasavyo Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi yenye lengo la
kuleta usawa na maendeleo endelevu kwa wananchi wote.
Aidha, uongozi huo walieleza kuwa wengi wa waajiri
wa sekta binafsi wametekeleza agizo la wafanyakazi la kuwaongezea mishahara
kwani hizo ni haki za wafanyakazi na wamekuwa wakizisimamia kwa nguvu zote.
Pia, walieleza kuwa na mashirikiano makubwa
sambamba na kufanya kazi kwa pamoja kati yao na Wizara ya Katiba na Sheria.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment