Habari za Punde

Waziri wa fedha aridhishwa na kasi ya ujenzi wa maduka Michenzani ( Shopping Mall)

Na Ali Issa    Maelezo     
Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Mohammed Ramia Abdiwawa amesema ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa maduka unaoendelea katika eneo la michezani na maskani ya Kisonge mjini Zanzibar.
Hayo ameyasema leo huko Michenzani wakati aki  fanya ziara ya ukaguzi kuangalia maendeleo ya u jenzi wa maduka Mool shoop na Kisonge.
Amesema kuwa ameridhishwa na ujenzi huo kwa hatua  uliofikia  licha ya kuwa na changamoto ndogo ndogo zinazojitokeza katika ujenzi huo.
Akizitaja changamoto hizo kwa upande wa jengo la kisonge maskani linalo jengwa  na Chama cha Mapinduzi ikiwemo mchanga maalumu ambao wanauhitaji  wakati wa kujengea nguzo  pamoja na kokoto.
Aidha amesema Serikali tayari imezipatia ufumbuzi  changamoto hizo ambapo majengo hayo yanatarajiwa  kukamilika ifikapo mwaka 2020.
Hata hivyo amewataka vijana wa kizanzibari wachangamkie frusa ya ajira katika ujenzi unao endelea kwani hiyo ndio njia moja ya kupata kipato halali.
Nae mshauri elekezi wa maduka mall shop yanayo jengwa kwa udhamini wa ZSSF Rose Nestory alimwambia  Waziri jengo hilo litakuwa na ghorofa tisa, Ambalo litagharimu shilingi bilioni 27.9 hadi kukamilika kwake.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.