Afisa Mkuu wa Benki ya CRDB Bank.Ndg.Fredrick Nshekanabo akizungumza wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Huduma Mpya ya kutuma fedha kati ya Ezypesa na Simbanking kupitia Simu ya Mkono ya Zantel na Benki ya CRDB Tanzania,hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Madinat Al Bahri Mbweni Zanzibar.
Ndugu Mohamed Khamis Baucha, Mkuu wa Kampuni ya Zantel
Zanzibar,
Viongozi na wafanyakazi wa Zantel,
Wafanyakazi wenzangu wa Benki ya CRDB,
Waandishi wa Habari,
Mabibi na Mabwana.
Asalam Aleykhum,
Ndugu Mgeni Rasmi,
Awali ya yote naomba nitumie
nafasi hii kipekee kabisa kutoa shukrani zangu za dhati kwako, kwa kukubali
kujumuika nasi katika hafla hii fupi ya uzinduzi huduma ya kutuma pesa
kidigitali kutumia simu ya mkononi kati ya Eazypesa na SimBanking ya CRDB bank.
Asante sana
Kipee kabisa nichukue fursa
hii kuwashukuru viongozi wa kampuni ya ZANTEL kwa kushirikiana nasi katika
kufanikisha jambo hili. Asanteni
sana!
Pia niwashukuru na kuwakaribisha viongozi mbalimbali
wa Serikali na wageni wote ambao wamejumuika nasi katika hafla hii. Karibuni
sana!
Ndugu Mgeni Rasmi,
Dira ya Benki yetu ya CRDB
inalenga katika kutoa huduma bunifu na zenye kukidhi mahitaji ya wateja wetu, popote
walipo.
Siku zote, tunaamini katika
kuongeza njia mbadala za kutolea huduma zetu ili tuweze kuwafikia wananchi
wengi zaidi. Kwa kurahisisha upatikanaji wa huduma zetu, tumesaidia kuingiza
wananchi wengi zaidi katika mfumo rasmi wa malipo, na hivyo kuchochea ukuaji wa
uchumi kwa mwananchi mmoja mmoja na nchi nzima kwa ujumla.
Ndugu Mgeni Rasmi,
Tukiongozwa na kauli mbiu isemayo “Benki
inayomsikiliza Mteja”, mwaka 2011, tuliingiza sokoni mfumo wa utoaji
huduma kupitia simu za mkononi ujulikanao kama “Simbanking”. Kupitia huduma hii mteja anaweza kufanya yafuatayo:
·
Kupata
taarifa fupi za akaunti yake,
·
Kuangalia
salio,
·
Kufanya
malipo ya Ankara (Luku, Dstv, Azam TV, n.k)
·
Kununua
muda wa maongezi
·
Kupata
mkopo wa haraka wa mshahara (Salary Advance)
·
Kuhamisha
pesa kwenda benki nyingine na mitandao ya simu
·
Kufanya malipo
ya serikali kupitia mfumo wa kielektroniki wa Serikali (GePG)
Ndugu Mgeni Rasmi,
Huduma hii ya SimBanking inapatikana kwa kwa njia mbili:
·
Kwanza
kupiga *150*03# na kufuata maelekezo
·
Pili
kupitia “SimBankingApp” inayoweza
kupakuliwa kupitia mtandao wa intaneti.
Ndugu Mgeni Rasmi,
Huduma
ya SimBanking ambayo
mpaka sasa inatumiwa na zaidi ya wateja milioni mbili, inalenga kuwapa wateja
wetu urahisi “convenience” wa kufanya
miamala yao popote walipo na kwa wakati wautakao, ndio maana tumekuwa tukitumia kauli mbiu ya “Ulipo Tupo”.
Ndugu Mgeni Rasmi,
Takwimu zinaonyesha ni
asilimia 60 ya watanzania ndio wameunganishwa na mfumo wa kifedha kupitia simu
za mkononi, wakati ni asilimia 17 tu ya watanzania ndio wanaotumia huduma za
kibenki. Hii inaonyesha kuwa njia rahisi zaidi ya kufikisha huduma za kifedha
kwa wananchi, ni kupitia simu zao za mikononi.
Hivyo basi, kuungana kwa Benki
ya CRDB na Kampuni ya Zantel kupitia huduma hizi za SimBanking na Eazypesa, ni
sehemu ya mkakati huo.
Ndugu Mgeni Rasmi,
Benki ya CRDB ina furaha
kuanza kushirikiana na kampuni ya simu ya Zantel na kuzindua rasmi upatikanaji
wa huduma za Eazypesa kupitia mfumo wa SimBanking. Muunganiko huu pia, utawapa
wateja wa benki ya CRDB wenye kutumia mtandao wa Zantel, uwezo wa kuzifikia
akunti zao kupitia simu zao za mikononi, hivyo kuwaondolea ulazima wa
kutembelea matawi yetu pindi wanapohitaji huduma. Kwa kiasi kikubwa, muunganiko
huu utasaidia kufikisha huduma za kifedha kwa watanzania wengi zaidi na kwa
urahisi zaidi.
Kwa kuanzia, huduma zifuatazo
zitapatikana:
·
Kuhamisha fedha kutoka akaunti ya
CRDB kwenda Eazy-Pesa
·
Kuhamisha fedha kutoka Easzypesa
kwenda akaunti yoyote ya CRDB
·
Kununua muda wa maongezi kupitia
Simbanking
Tutaendelea kuboresha upatikanaji wa huduma hizi
ili kuondoa kabisa ulazima wa wateja wetu kutembelea mabenki hivyo kuwapa muda
wa kujikita kwenye shughuli za uzalishaji mali na ujenzi wa taifa.
Ndugu Mgeni Rasmi, wageni waalikwa.
Nimalize kwa kuwashukuru wote kwa kufika na kuungana nasi kwenye hafla
hii ya uzinduzi. Pia nitoe rai kwenu waandishi wa habari kuwaelimisha na
kuwafikishia ujumbe wateja wetu na watanzania kwa ujumla juu ya upatikanaji wa
huduma hii.
Aidha, naomba niwakaribishe
watanzania wote kuendelea kufurahia huduma za Benki ya CRDB kupitia mtandao
wetu uliosambaa nchi nzima bara na visiwani. Nimalize kwa kusema “ULIPO TUPO” tupo tayari kukuhudumia.
Asanteni
kwa kunisikilia
No comments:
Post a Comment