MKE
wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein akishuhudia huduma ya Upimaji wa Afya kwa Wazee wa Sebleni na Welezo ikitolewa
na Daktari Bingwa kutoka Jamuhri ya Watu wa China.Dr.Yang Xiaodong akimpima presha Bi.Nagawiya Ramadhani,wakati wa
uzinduzi huo uliofanyika katika ukumbi wa nyumba za Wazee Sebleni Wilaya ya Mjini Unguja, (kulia
kwa Mama Mwanamwema Shein) Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.Mama Asha
Suleiman Iddi
MKE wa Rais wa Zanzibar, mama
Mwanamwema Shein amesema kwa kuzingatia umuhimu wa wananchi kuwa na afya bora,
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeweka kipaumbele katika sekta ya Afya, kwa
kuimarisha huduma mbali mbali .
Mama Mwanamwema amesema hayo katika
uzinduzi wa huduma za upimaji afya kwa wazee wanaoishi katika nyumba za wazee
Sebleni na Welezo, hafla iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano Sebleni, mjini
hapa.
Timu ya madaktari bingwa kutoka
Jamuhuri ya watu wa China, wakishirikiana na madaktari wazalendo wameendesha
zoezi la upimaji wa Afya kwa wazee wanaoishi katika nyumba hizo na kutoa huduma
za uchunguzi, dawa na ushauri.
Alisema ili kufanikisha dhamira hiyo,
Serikali imechukuwa hatua mbali mbali, ikiwa pamoja na kuimarisha miundombinu,
kununua vifaa vya kisasa vya uchunguzi,
kuongeza bajeti ya dawa, kuongeza madaktari pamoja na kusomesha vijana wake
ndani na nje ya nchi.
Alisema hivi sasa huduma za za Afya
katika hospitali na vituo vya Afya kote nchini zimeimarika na kutolewa bure , ikiwa ni hatua ya
kufanikisha malengo ya muasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar, marehemu mzee Abeid
Amani Karume.
Alieleza kuwa hatua ya washirika wa maendeleo, ikiwemo Jamuhuri ya
Watu wa China, kuunga mkono juhudi hizo kwa wataalamu wake kupima afya za wazee
hapa nchini, ni jambo la kutia moyo na linalopasa kupongezwa.
“Kuwapima afya wazee wetu ni kuendeleza
jitihada za kuwaenzi na kuwahudumia wazee wetu, hakika wazee hawa walifanya kazi ya kutulea na kuijenga nchi
yetu, hii ni kuonyesha tunawathamini, tunawajali na tunawapenda”, alisema.
Aliwataka wazee hao kuitumia vyema
fursa waliyoipata na kutoa ushirikiano kwa wataalamu hao, ili kufikia malengo
yaliokusudiwa.
Aidha, alitowa wito kwa wazazi na walezi kote nchini kusimamia
vyema malezi ya watoto wao kwa kuzingatia maadili mema, utamaduni na silka za Wazanzibari, ili hatiame waweze
kuwa raia wema.
Mama Mwanamwema alisitiza haja ya
kuwahimiza watoto kuzingatia masomo yao ya skuli na madrasa pamoja na
kuwafuatilia nyendo zao ili kuwaepusha na vitendo viovu, udhalilishaji na
matumizi ya dawa za kulevya.
Alitowa shukrani kwa timu hiyo ya
madaktari kwa mara ya pili kukubali kutoa huduma za upimaji wa afya, hatua
aliyobainisha inaonyesha mapenzi makubwa na urafiki uliopo kati ya wananchi wa
China na Zanzibar.
Aidha, mama Mwanamwema alitowa ombi
maalum kwa Ubalozi mdogo wa China uliopo Zanzibar akiomba huduma hizo zifikishwa
kisiwa Pemba kwa ili wazee wanaoishi katika nyumba za wazee Limbani, nao waweze
kufaidika.
Altowa pongezi kwa Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein kwa kutimiza miaka tisa
ya uongozi wake na kubainisha maendeleeo makubwa ya kiuchumi na kijamii yaliofikiwa.
Mapema, Mke wa Makamo wa Pili wa Rais
wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Idd, aliwashukuru madaktri hao kwa moyo wao wa kujitolea
na kuona umuhimu wa kuwaenzi na kuwahudumia wazee wa Zanzibar.
Aidha, aliishukuru Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar, chini ya Chama cha Mapinduzi kwa kuwajali na kuwathamini
wazee.
Nae, Waziri wa Kazi, Uwezeshaji,
wazee, wanawake na watoto, Moudline Castico alipongeza juhudi endelevu za Mama
Mwanamwema na Mama Asha Suleiman , ambapo kwa nyakati tofauti wamekuwa mstari wa
mbele kutoa misada mbali mbali ya kijamii kwa wazee na watoto wanaolelewa
katika nyumba za Serikali.
Alisema wazee wamekuwa wakikabiliwa na
magonjwa mbali mbali, ikiwemo sukari, shinikizo la damu, kiharusi, macho,
masikio na mengineyo, hivyo akabainisha hatua ya Ubalozi wa China kuedesha
zoezi hilo kuwa ni ya kupongezwa.
Alimpongeza Mke wa Balozi mdogo wa Jamuhri ya Watu wa China Zanzibar.Bi Liu Jie kwa juhudi kubwa alizochukuwa kufanikisha kazi ya kuwapima afya
wazee, hatua aliyoeleza inayonesha imani na mapenzi kwa wazee hao.
Aidha, Mke wa Balozi mdogo wa China
aliopo Zanzibar, Liu Jie aliipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, chini
ya uongozi wa Dk. Shein kwa juhudi mbali mbali inazozichukuwa kudumisha amani
na kuimarisha uchumi.
Alisema China itaendelea kuiunga mkoni
Zanzibar katika dhamira zake za
kuimarisha uchumi, sambamba na kuendeleza mashirikiano yaliopo kati ya nchi
mbili hizo.
Alisema ushirikiano kati ya China na
Zanzibar ni wa kihistoria, hivyo akaahidi kuendelezwa na kubainisha upimaji wa afya
kwa wzee hao ni hatua inayoonesha heshima na upendo.
Nao, wazee mbali mbali waliopatiwa
huduma hizo, wameishukuru Serikali, Ubalozi mdogo wa China pamoja na Mke wa
Rais wa Zanzibar kw akufanikisha zoezi hilo muhimu.
Wamesema wamefurahishwa kupata fursa
hiyo, kwani imemwawezesha kueleeza changamoto mbali mbali za maradhi
yanayowakabili na kuchunguzwa na hatiame kupata dawa na ushauri wa kitaalamu.
Katika hafla hiyo
Mke wa Balozi wa China aliopo nchini Bi Liu Jie aliikabidhi zawadi na vifaa
mbali mbali kwa wazee wanaoishi nyumba za wazee Welezo na Sebleni.
Nyumba za
kutunzia wazee ziliopo Welezo na Sebleni
zina jumla ya wazee 71 wa kike na kiume, ambao hupatiwa huduma zote muhimu,
ikiwemo Chakula, malazi, matibabu na Serikali.
Abdi Shamna,
Ikulu Zanzibar
Postal
Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024 2231822
E-mail: abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment