Mtwakwimu Mkuu wa Serikali.Dkt.
Albina Chuwa akisisitiza kuhusu ushirikiano mzuri uliopo kati ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu
(NBS) na Benki ya Dunia, hayo yamejiri Oktoba 31, 2019 Jijini Dodoma wakati wa kikao
cha ujumbe huo na menejimenti ya NBS ilikufanikisha Mpango Kambambe wa Taifa wa Kuboresha na Kuimarisha Takwimu
(TSMP) awamu ya pili.
Na. Mwandishi Wetu
Serikali ya Awamu ya
Tano imetajwa kufanikiwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kutokana na
matumizi bora ya takwimu zinazozalishwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).
Akizungumza leo
Jijini Dodoma, Mtakwimu mkuu wa Serikali Dkt. Albina Chuwa amesema kuwa Ofisi
hiyo imefanikiwa kuzalisha takwimu zenye ubora wa viwango vinavyokubalika
kimataifa hali inayochochea mafanikio ya miradi inayotekelezwa ikilenga
kuchochea ustawi wa wananchi.
“Tunatarajia kujenga
Ofisi katika mikoa yote hapa nchini ili kuboresha zaidi mfumo wa ukusanyaji
takwimu kuiwezesha Serikali kupanga mipango yake kwa ufanisi mkubwa zaidi”
Alisisitiza Dkt. Chuwa
Akifafanua amesema kuwa takwimu bora ni msingi wa maendeleo
yaliyofikiwa hapa nchini katika sekta zote zinazolenga kuleta ustawi wa
wananchi.
Akizungumzia
utekelezaji wa mpango Kabambe wa Taifa wa Kuboresha na Kuimarisha Takwimu
(TSMP) awamu ya pili Dkt. Chuwa amesema kuwa unalenga kufanya maboresho zaidi
katika ukusanyaji na uchakataji wa takwimu kwa kujenga miundombinu bora zaidi
hadi ngazi ya mikoa ikiwemo majengo.
“Lengo namba 17 la
Malengo ya Millenia linasisitiza ushirikiano kati ya Serikali na wadau ili
kuchochea maendeleo ya wananchi ndio maana tumekuwa na ushirikiano huu na Benki
ya Dunia” Alisisitiza Dkt Chuwa
Kwa upande wake
mchumi mwandamizi kutoka Benki ya Dunia Bi. Bi Nadia Belhaj Hassine Belghith
amesema kuwa Tanzania ni nchi ya kupigiwa mfano kwa maendeleo yaliyofikiwa
katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu, afya, miundombinu na nyingine kutokana
na matumizi ya takwimu zenye viwango na ubora unaotakiwa.
“Takwimu
zinawawezesha wakulima kujua wapi yalipo masoko ya mazao yao hivyo kuchochea
maendeleo yao na nchi kwa haraka zaidi” Alisisitiza Bi. Belghith
Akifafanua amesema
kuwa takwimu ni msingi na kichocheo cha maendeleo katika Taifa lolote kama
ilivyo kwa Tanzania ambayo katika Afrika ni ya pili kwa kuzalisha Takwimu Bora.
Ujumbe wa Benki ya
Dunia na Ofisi ya NBS wamekutana Jijini Dodoma kwa wiki moja katika mkutano wa mashauriano
wa kuimarisha ushirikiano wao. Katika mkutano huo moja ya masuala
yaliyozungumziwa ni kufanikisha utekelezaji wa Mpango Kabambe wa Pili wa Taifa
wa Kuboresha na Kuimarisha Takwimu (TSMP II) unaotarajiwa kutekelezwa kwa
kipindi cha miaka 5 kuanzia 2019/ 2020 hadi 2024/ 2025 baada ya kumalizika kwa
mpango kama huo mwezi Juni mwaka jana.
No comments:
Post a Comment