Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na wadau wa Tija katika Ukumbi wa HAZINA Ndogo jijini Dodoma wakati akifungua mkutano wa wadau hao kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wenye lengo la kujadili uboreshaji wa utendaji kazi katika Utumishi wa Umma ili kuongeza Tija.
Baadhi ya wadau wa Tija wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) katika Ukumbi wa HAZINA Ndogo jijini Dodoma wakati akifungua mkutano wa wadau hao kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wenye lengo la kujadili uboreshaji wa utendaji kazi katika Utumishi wa Umma ili kuongeza Tija.
Na.James
K. Mwanamyoto.
Wadau wa tija katika
Utumishi wa Umma pamoja na wanazuoni
wametakiwa kujadili na kuishauri Serikali juu ya namna bora ya kuboresha
utendaji kazi na kuongeza Tija Serikalini.
Wito huo umetolewa
jijini Dodoma leo, na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) wakati akifungua mkutano wa
wadau kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wenye lengo la
kujadili uboreshaji wa utendaji kazi katika Utumishi wa Umma ili kuongeza Tija.
Dkt. Mwanjelwa
amesema, mchango wa wadau hao utasaidia kuishauri Serikali namna ya kuboresha utendaji kazi kwa watumishi wa umma
na kuongeza tija ambayo itasaidia katika
kutoa huduma bora kwa wananchi ambao ndio walengwa wa maendeleo na huduma zenye
kiwango stahiki zinazotakiwa kutolewa na Taasisi za Umma.
“Nawasihi mjikite
zaidi katika kuchambua na kutafakari kwa kina juu ya namna ya kuwa na misingi
imara na vigezo vitakavyosaidia katika kuboresha zaidi utendaji kazi Serikalini
na kuongeza Tija”, amesisitiza Dkt. Mwanjelwa.
Aidha, Dkt. Mwanjelwa
ameongeza kuwa, ongezeko la pato la taifa lolote duniani ndio msingi na chanzo
cha kuboresha mishahara na masilahi ya watumishi, kuboresha maisha na kuwaletea
maendeleo wananchi wake, hivyo wadau wanapaswa kuishauri vema Serikali kuongeza
wigo wa mapato na hatimaye iweze kuboresha masilahi ya watumishi wa umma.
Mkutano huu wa siku
mbili wa wadau wa kujadili uboreshaji wa utendaji kazi katika Utumishi wa Umma
ili kuongeza Tija umeratibiwa na Bodi ya Mishahara na Masilahi katika Utumishi
wa Umma kwa lengo la kuiwezesha Serikali kupata mchango na ushauri katika
kuboresha utendaji kazi na Tija ndani ya Utumishi wa Umma.
No comments:
Post a Comment