Habari za Punde

Tanzania Kuadhimisha Siku ya Wanawake wa Afrika Kuadhimishwa Julai 31 Kila Mwaka.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akimkabidhi kitenge cha Siku ya Wanawake Duniani kwa mwaka huu Mtangazaji wa Zamani wa Redio Tanzania Bibi. Deborah Mwenda baada ya kufungua mkutano wa waasisi wa Umoja wa Jumuiya za Wanawake katika nchi huru za Afika (PAWO) tawi la Tanzania na Wizara uliolenga kutoa maoni yao katika uboreshaji wa Sera ya Maendeleo ya Wanawake na Jinsia uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu Dar Es Salaam
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amewataka watendaji wa Wizara yake upande wa Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii kuizingatia tarehe 31 mwezi Julai kila mwaka na kuhakikisha Tanzania inaadhimisha Siku za Wanawake wa Afrika.
Waziri Ummy ameyasema hayo leo Jijini Dar Es Salaam wakati wa mkutano na waasisi wa Umoja wa Jumuiya za Wanawake katika nchi huru za Afika (PAWO) tawi la Tanzania walipokutana na Wizara katika kutoa maoni yao katika uboreshaji wa Sera ya Maendeleo ya Wanawake na Jinsia.
Waziri amesema kuwa Tanzania ni miongoni mwa mataifa yaliyo mstari wa mbele katika kukuza usawa wa kijinsia na kuwezeha wanawake katika Nyanja mbalimbali hivyo ni muhmu kwa taifa kuadhimisha Siku ya Wanawake wa Afrika ili kuongeza nguvu katika jitihada hizo za Serikali.
“Kwa kuzingatia haya ndio maana kama Serikali tumetoa kipaumbele katika masuala ya kukuza usawa wa kijinsia na kuiweka kuwa ni miongoni mwa ajenda muhimu za maendeleo za kitaifa na utekelezaji wake utagusa Nyanja mbalimbali” Alisema.
Ameongeza kuwa pia msukumo mkubwa umewekwa na Serikali katika suala la kuhusisha masuala ya kijinsia katika Sera, Mikakati, na Programu za kisekta na kitaifa, uwezeshaji wanawake na kuzuia na kutokomeza ukatili wa kijinsia.
“Serikali imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kuwa wanawake wanapata fursa ya kushiriki kwenye ngazi mbalimbali za maamuzi na uongozi katika nyanja za kiuchumi, kijamii an kisiasa” alisema.
Waziri amesisitiza kuwa jitihada zote hizo zisingeweza kutekelezwa kama kusingekuwa na Umoja wa Jumuiya za Wanawake katika nchi huru za Afrika (PAWO) kwani wananchama wake wamekuwa wakijitolea kuongoza jitihada hizi kwa umoja na mshikamano ili kuleta uhuru, amani, haki na utengamano kwa watu wa Afrika hasa wanawake.
“Hii yote imewezesha nchi za Umoja wa Afrika ikiwemo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuweka mazingira wezeshi kwa wanawake ambayo leo hii tunaona matunda yake” alisema
Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Maendeleo ya Jinsia Bi. Grace Mwangwa amesema kuwa ushiriki wa waasisi hao katika mkutano huo utasaidia katika kupata uzoefu katika nyanja walizokuwa wakizifanyia kazi katika kuleta amani, utulivu, na kuleta usawa wa kijinsia na ustawi na maendeleo ya wanawake na wasichana nchini.
Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Jumuiya za Wanawake katika nchi huru za Afrika (PAWO) Bibi. Leah Lupembe ameishukuru Serikali kwa kuona umuhimu wa kuadhimisha Siku ya Wanawake wa Afrika kila Julai 31 kwani itasaidia jamii ya watanzania kuelewa kuhusu mapambano na mchango wa wanawake wa Afika katika uhuru na kuwezesha wanawake kupata fursa sawa katika nyanja mbalimbali.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akizungumza wakati mkutano na waasisi wa Umoja wa Jumuiya za Wanawake katika nchi huru za Afika (PAWO) tawi la Tanzania walipokutana na Wizara uliolenga kutoa maoni yao katika uboreshaji wa Sera ya Maendeleo ya Wanawake na Jinsia uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akisalimiana na Prof. Marjone Mbilinyi wakati wa mkutano na waasisi wa Umoja wa Jumuiya za Wanawake katika nchi huru za Afika (PAWO) tawi la Tanzania walipokutana na Wizara uliolenga kutoa maoni yao katika uboreshaji wa Sera ya Maendeleo ya Wanawake na Jinsia uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akiangalia picha ya pamoja na waasisi wa Umoja wa Jumuiya za Wanawake katika nchi huru za Afika (PAWO) tawi la Tanzania wakati wa mkutano na Wizara uliolenga kutoa maoni yao katika uboreshaji wa Sera ya Maendeleo ya Wanawake na Jinsia uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akiwa na mmoja wa Muasisi wa PAWO Bibi.Tecla Sumbo mara baada ya kufungua mkutano wa waasisi wa Umoja wa Jumuiya za Wanawake katika nchi huru za Afika (PAWO) tawi la Tanzania na Wizara uliolenga kutoa maoni yao katika uboreshaji wa Sera ya Maendeleo ya Wanawake na Jinsia uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya waasisi wa Umoja wa Jumuiya za Wanawake katika nchi huru za Afika (PAWO) tawi la Tanzania wakiwa na vitenge vya Siku ya Wanawake Duniani kwa mwaka huu  mara baada ya kufungua mkutano wao na  Wizara uliolenga kutoa maoni yao katika uboreshaji wa Sera ya Maendeleo ya Wanawake na Jinsia uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya waasisi wa Umoja wa Jumuiya za Wanawake katika nchi huru za Afika (PAWO) tawi la Tanzania mara baada ya kufungua mkutano na Wizara uliolenga kutoa maoni yao katika uboreshaji wa Sera ya Maendeleo ya Wanawake na Jinsia uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Picha Zote na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WAMJW

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.