Habari za Punde

Timu ya Kajengwa Yanyakua Ngao ya Hisani ya Michuano ya Yamleyamle ZBC 2020 Kwa Kuifunga Timu ya Uzi City Bao 3-1.Mchezo Uliofanyika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar.

Mshambuliaji wa Timu ya Uzi City mwenye mpira Abdul  Warith  akiwapita mabeki wa Timu ya Kajengwa (kulia) Aseed Abdalla na (kushoto)Abra Abdalla wakati wa mchezo wa ufunguzi wa Michuano ya Yamleyamle ZBC 2020 mchezo wa Ngao ya Hisani uliofanyika katika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar.Timu ya Kajengwa imeshinda mchezo huo kwa bao.3-1.
Mshambuliaji wa Timu ya Uzi City Abdul Warith akimpita beki wa Timu ya Kajengwa Aseed Abdalla wakati wa mchezo wa ufunguzi kuwania Ngao ya Hisani ya Yamleyamle ZBC 2020, mchezo uliofanyika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar. Timu ya Kajengwa imeibuka mshinda na kukabidhiwa Ngao ya Hisani kwa ushindi wa bao 3 -1.  
Mchezaji wa Uzi City na Kajengwa wakiwania mpira ukiwa juu wakati wa mchezo wao wa Ngao ya Hisani ya ufunguzi wa michuano ya Yamleyamle ZBC 2020, mchezo uliofanyika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar Timu ya Kajengwa imeibuka mshindi kwa bao 3-1.







No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.