Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James
(kushoto), akisaini Mikataba mitano yenye thamani ya Dola za Marekani 495.59 na
Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo
Afrika (AfDB), Alex Mubiru (kulia) katika hafla iliyofanyika Benki Kuu Jijini
Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James
(kushoto), akibadilishana nakala ya Mkataba na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB),
Alex Mubiru (kulia) katika hafla iliyofanyika Benki Kuu Jijini Dar es Salaam,
Tanzania na AfDB zimesaini mikataba mitano yenye thamani ya Dola za Marekani
495.59.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James,
akiwa katika picha ya pamoja na Katibu
Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Mawasiliano (Ujenzi), Mhandisi Elius Mwakalinga (wa
pili kushoto), Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika(AfDB), Alex Mubiru(
wa pili kulia), Afisa Mtendaji Mkuu Tanroad, Patrick Mfugale na watendaji wa
Mamlaka Viwanja vya Ndege na Tanroad mara baada ya utiaji saini wa mikataba ya
Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege wa Kimaifa wa Msalato Jijini Dodoma, Ujenzi wa Barabara
ya Bagamoyo-Pangani-Tanga uliofanyika katika Ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania,
Jijini Dar es Salaam.
Na.Mwandishi
Wetu-MAELEZO
Serikali ya Tanzania
na Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), zimesaini mikataba mitano ya mkopo wa
masharti nafuu ya Dola za Marekani milioni 495.59 ambayo ni sawa na TZS
trilioni 1.14 zitakazowezesha kutekeleza ujenzi wa miradi ya Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa Msalato Jijini Dodoma, Dola za Marekani milioni 271.63, ujenzi wa barabara ya
Bagamoyo-Holoholo-Lungalunga–Malindi km.120.8 kwa gharama ya Dola za Marekani milioni
168.76 na Dola 55.2 kwa ajili ya Programu ya utawala bora na kuendeleza Sekta
Binafsi.
Katika hafla ya
utiaji saini iliyofanyika katika Ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania Jijini Dar es
Salaam, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James alisema kuwa
Serikali ya Tanzania na Benki ya Maendeleo Afrika zimekuwa na mahusiano mazuri
ambayo yamewezesha kutolewa kwa mkopo huo wenye masharti nafuu.
“Kama tunavyojua sekta
ya miundombinu ndiyo sekta muhimu ambayo inaweza kuinua biashara na kukuza
uchumi kwa hiyo katika kulitambua hilo Benki ya Maendeleo Afrika imekubali
kutupatia mkopo huu, ambao utatumika katika utekelezaji wa kuboresha miundombinu
kwa ujenzi wa Uwanja mkubwa wa Ndege Msalato Jijini Dodoma utawezesha kumudu
ndege kubwa za kimataifa kutua”, alisema Doto James.
Alisema kuwa kupitia
mikataba hiyo AfDB itaipatia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mikopo
ya masharti nafuu ya dola za Marekani milioni
198.63 kupitia dirisha la African
Davelopment Bank ( ADB Window), dola Marekani milioni 246.96 kupitia African Development Fund (ADF Window) na
dola milioni 50 kupitia mfuko wa Serikali ya China unaosimamiwa na AfDB.
Aliongeza kuwa ujenzi
wa Uwanja wa Ndege Msalato na ujenzi wa barabara ya Bagamoyo-Pangani kwa
kiwango cha lami itaisaidia Serikali kuziba pengo la miundombinu na kuchochea
kasi ya maendeleo ya Uchumi kwa jamii ya watanzania.
Aidha kupitia AfDB
miundombinu ya barabara mbalimbali imeshatekelezwa na zinaendelea kutekelezwa
zikiwemo za Tabora-Koga-Mpanda Km 342.9, Mbinga-Mbamba bay Km. 66, mradi wa
awamu ya pili ya mabasi yaendayo kasi Km. 20.3, Kabingo-Kasulu-Manyovu Km. 260,
barabara ya kuzunguka Jiji la Dodoma Km.110.2 huku upande wa Zanzibar AfDB
inafadhili barabara za Bububu-Mahonda-Mkokotoni Km.31 na barabara za
kuunganisha vijiji vya Zanzibari Km.21, kwa hiyo benki hii ni wadau wakubwa wa
maendeleo Tanzania
Pia Alibainisha kuwa
kuna barabara nyingi za ufadhili kutoka Benki ya Maendeleo Afrika zimekamilika
na kutumiwa na wananchi kufanya biashara na kukuza uchumi wao zikiwemo za
Arusha-Namanga km. 105, Singida-Babati-Minjiru km. 223.5, Iringa Dodoma km.260,
Tunduru-Mangaka-Mtambaswala km.202.5, Namtumbo-Tunduru km.193 Dodoma-Babati
km.188.1 na Arusha bypass km.42.4 pamoja na upanuzi wa barabara ya
Sakina-Tengeru km 14.1 kwa njia nne kwa hiyo ushirikiano huu umewezesha
kuimarisha ujenzi wa miundombinu hiyo ili kumarisha sekta ya usafirishaji.
Naye Mwakilishi Mkazi
wa Benki ya Maendeleo Afrika AfDB nchini Tanzania, Bw. Alex Mubiru, alisema
kuwa mikataba hiyo inayotoa dola za Marekani 495.6 zitafikisha dola za Marekani
bilioni 2.38 ambapo kati ya hiyo dola za Marekani bilioni 1.47 zimewekezwa
kwenye miradi ya miundombinu.
“Ujenzi wa Uwanja wa
Ndege Msalato utachukua takribani miaka minne ambapo inakadiliwa kuwa na uwezo
wa kubaba ndege 50, 000 kwa mwaka, abiria 1.5 na utakuwa uwanja mkubwa wa
kimataifa Jijini Dodoma utakatumiwa na zaidi ya watu milioni 200 duniani kote
wafanyabiashara na watalii”, Alisema Alex Mubiri.
Kwa upande wake Afisa
Mtendaji Mkuu wa Tanroad, Mhandisi Patrick Mfugale alisema kuwa ujenzi wa
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Msalato Jijini Dodoma utakuwa na uwezo wa Kutosha
kubeba ndege kubwa kwani utakuwa na urefu wa kilomita 3.6 na upana wa mita 60.
“Uwanja huu wa
Msalato Jijini Dodoma utakuwa mkubwa wa kuhudumia ndege kubwa aina ya
Dreamliner 17, na kama ni aina ya Airbus ni ndege 380, magari ya kawaida 472, na mabasi ya abiria 72, na
ukimalizika utahudumia abiria mililioni 1.5 kwa mwaka”, alisema Mhandisi
Mfugale.
Lakini pia ujenzi wa
daraja la mto pangani utasaidia wananchi wa Tanga kufanya biashara zao bila
usumbufu ambapo daraja hilo litakuwa na nguzo nane, huku barabara ikiwa na km
105 barabra kuu na km. 25 barabara unganishi.
No comments:
Post a Comment