Habari za Punde

WAZIRI SIMBACHAWENE AWAONGOZA WATENDAJI WA WIZARA KIKAO CHA KAMATI YA BUNGE KUWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA BAJETI, BUNGENI JIJINI DODOMA

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kushoto), akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini, Hasna Mwilima, nje ya Ukumbi wa Bunge, jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ndani ya Nchi, Ramadhani Kailima, akijipaka kitakasa mikono (Sanitizer) nje ya Ukumbi wa Bunge, jijini Dodoma, leo, kabla ya kuanza kwa Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Pius Msekwa.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene akizungumza katika Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Pius Msekwa, Bungeni jijini Dodoma, leo. Wizara iliwasilisha katika kikao hicho Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2020/21. Katikati ni Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Salim Mwinyi Rehani, na kulia ni Katibu wa Kamati hiyo, Ramadhani Abdalla.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Christopher Kadio (kulia), na Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Wanja Mtawazo, wakipanga nyaraka kwa ajili ya kuziwasilisha katika Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Pius Msekwa, Bungeni jijini Dodoma, leo. Wizara iliwasilisha katika kikao hicho Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2020/21. 
Wakuu wa Idara wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakimsikiliza Waziri wa Wizara hiyo, George Simbachawene (hayupo pichani) alipokuwa anazungumza katika Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Pius Msekwa, Bungeni jijini Dodoma.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kushoto) akimsikiliza Katibu wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Ramadhani Abdalla (kulia) alipokuwa anamfafanulia jambo kabla hya kuanza kwa Kikao cha Kamati hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Pius Msekwa, Bungeni jijini Dodoma, leo. Watatu kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Christopher Kadio, na wapili kushoto ni Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Wanja Mtawazo.
Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.  

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.