Habari za Punde

WAZIRI BASHUNGWA AMEWAAGIZA TEMDO KUTENGENEZA MASHINE ZA KUKAMUA MIWA NA KUCHAKATA ZAO LA MKONGE.

Waziri wa Viwanda na Bishara Mhe Innocent Bashungwa akikagua bidhaa za wajasiriamali wadogo zinazochakatwa na mashine zilizotengenezwa na Taasisi ya Uhandisi na Usanifu wa Mitambo Tanzania (TEMDO) - Arusha, 25 Aprili 2020.

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa ametoa rai kwa Taasisi ya Uhandisi na Usanifu wa Mitambo Tanzania (TEMDO) kuhakikisha wanawasaidia wajasiliamali wadogo  na wa kati kubuni  mashine za kutengeneza sukari pamoja na kuchakata katani ili kufungua fursa ya ajira na ongezeko la viwanda nchini.

Mhe. Bashungwa aliyasema hayo mkoani Arusha alipokuwa akizindua mashine 14 za kisasa zinazoendeshwa kwa mfumo wa kompyuta yaani CNC zikiwa na  thamani ya shilingi milioni 600 zilizotolewa kwa fedha za Maendeleo za Serikali na za ufadhili wa shirika la kimataifa la UNIDO.

Akizungumza na watumishi wa taasisi hiyo Mhe. Bashungwa aliwataka TEMDO kuongeza kasi ya kubuni mtambo mdogo wa kuchakata miwa ili kupata sukari ili kuongeza uzalishaji na upatikanaji wa wa bidhaa hiyo sokoni.

Aliongeza kwa kusema wafanyabiashara wanapandisha bei ya bidhaa hususani sukari sokoni, lakini endapo TEMDO itatengezeza mashine za kutengeneza sukari kwa wajasiriamali wadogo  itawasaidia kujikwamua kiuchumi na kusaidia upatikanaji wa sukari nchini.

Aidha amewataka pia kuongeza kasi ya kubuni mashine  ndogo ndogo za kuchakata zao la mkonge kwa kiwango cha upatikanaji wa nyuzi ili kuwasaidia wajasiliamli wadogo kutengeneza nyuzi wao wenyewe ili waweze kuziuza na  kujiongezea kipato badala ya hali ilivyo hivi sasa ambapo wakulima wanategemea wazalishaji wakubwa kununua bidhaa hiyo kwa kiasi kikubwa ambapo mkulima amekuwa hanufaiki.

Sambamba na hilo Mhe. Bashungwa alikabidhi barakoa zenye thamani ya Tsh.500,000 zilizotolewa na TEMDO  kwa mkoa wa Arusha ikiwa ni sehemu ya kuungana na Serikali kupambana na ugonjwa wa Korona kwa watoa huduma ya afya.
Awali Mkurugenzi Mkuu wa TEMDO, Prof. Fredrick Kahimba aliishukuru serikali kwa kuwawezesha kupata mashine hizo ambazo zitawezesha kuunda mitambo na mashine mbalimbali kwa urahisi zaidi kuliko awali.

Aliongeza kuwa “taasisi ya TEMDO imeendeleza shughuli mbalimbali zinazochangia maendeleo ya Viwanda Tanzania na kuwawezesha wakulima na wajasiliamali wadogo, wa kati na wakubwa kujipatia teknologia ya kuogeza uzalishaji mali.
Pia alimuomba Waziri Bashungwa kusaidia kuharakishwa uundwaji wa bodi mpya ya Wakurugenzi ya taasisi kwa kuwa liyokuwepo imemaliza muda wake.

Kwa upande wake bi Restuta Mrosso ambaye ni mnufaika wa utaalamu unaotolewa na TEMDO aliishukuru taasisi hiyo kwa kuwapatia ujuzi  wajasiriamali kutengeneza bidhaa mbalimbali na kuwasaidia kupata nembo ya Ubora (TBS).
 Waziri wa Viwanda na Bishara Mhe Innocent Bashungwa {katikati} akikata utepe wa kuzindua mashine 14 za kisasa zinazoendeshwa kwa mfumo wa kompyuta yaani CNC zikiwa na  thamani ya shilingi milioni 600 zilizotolewa kwa fedha za Maendeleo za Serikali na za ufadhili wa shirika la kimataifa la UNID  {kulia} Mkurugenzi Mkuu wa TEMDO, Prof. Fredrick Kahimba, {kushoto}  Afisa biashara mka wa Arusha
Waziri wa Viwanda na Bishara Mhe Innocent Bashungwa akiongea na uongozi na menejimenti ya Taasisi ya Uhandisi na Usanifu wa Mitambo Tanzania (TEMDO) kabla ya uzindua mashine 14 za kisasa zinazoendeshwa kwa mfumo wa kompyuta yaani CNC zikiwa na  thamani ya shilingi milioni 600 zilizotolewa kwa fedha za Maendeleo za Serikali na za ufadhili wa shirika la kimataifa la UNID.- Arusha
Waziri wa Viwanda na Bishara Mhe Innocent Bashungwa {kulia} akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi Mkuu wa TEMDO, Prof. Fredrick Kahimba, {kushoto} kutengeneza mashine ndogo za  kukamua miwa ili kutengeneza Sukari ambayo itawasaidia wazalishaji wadogo na kati kuanza kuzalisha sukari  itakayosaidia nchi kuwa na utoshelevu wa mahitaji ndani ya sukari ili kufika malengo  mwaka 2024/25 kuzalisha sukari ya kutosheleza Watanzania pia na ziada kuuzwa  nje ya nchi.
Waziri wa Viwanda na Bishara Mhe Innocent Bashungwa akikikagua mtambo wa kuchomea taka za hospitali uliotengenezwa na Taasisi ya Uhandisi na Usanifu wa Mitambo Tanzania (TEMDO) - Arusha,
Mashine mpya za kisasa zinazoendeshwa kwa mfumo wa kompyuta yaani CNC zikiwa na  thamani ya shilingi milioni 600 zilizotolewa kwa fedha za Maendeleo za Serikali na za ufadhili wa shirika la kimataifa la UNID.- Arusha,

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.