Habari za Punde

Innaa lillaahi Wainnaa ilayhi Raajiuun: Bi Zuwena Salum mtangazaji wa kwanza wa kike sauti ya Unguja afariki

Bi Zuwena Salum ndiye aliyekuwa Mtangazaji wa kwanza wa kike Sauti ya Unguja na kwa Afrika Mashariki. 

Vipindi maarufu vya Bi Zuwena ni Ladies Club na Muungwana (kipindi kilichogusia Malezi ya Kizanzibari) Vipindi vya Mila, Desturi, Wema, Ihsani, khushui,  Akhlaqi na thaqafa za watu wa Visiwani.

Baadaye ndio wakaja Bi Sanura Juma Shakhsy na Zeyana Seif (BBC).

Mazishi yake yalikuwa leo Alkhamis tarehe 18 June 2020 hapo Wireless kwao.

Bi Zuwena alipata mtoto aitwaye Nabil.

Tumuombe Allah amsamehe makosa yake, amuweke mahala pema  peponi na awape subra wafiwa. 

Allaahumma  Amin

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.