MMOJA ya akinamama wanaotumia majiko sanifu kwa
kupikia, akipanga kuni katika jiko hilo ili kuweza kupikia, jiko ambalo ni
rafiki mkubwa wa mazingira.(PICHA NA
ABDI SULEIMAN)

MMOJA ya watumiaji wa majiko sanifu katika kupikia, aliyejulikana kwa jina la Asha Khamis akiongeza kuni katika jiko hilo, wakati alipokuwa akipika wali jiko sanifu ni rafiki mkubwa wa mazingira kwa kutokutumia kuni nyingi.(PICHA NA ABDI SULEIMAN
JIKO la mawe matatu ambalo hutumia kuni nyingi na
kuharibu mazingira kama linavyoonekana katika picha, katika siku za hivi
karibuni limekuwa likitoweka kutokana na uwepo wa majiko sanifu yan ayotumia
kuni kidogo na rafiki wa mazingira.(PICHA
NA ABDI SULEIMAN)
BAADHI ya mizigo ya kuni ikiwa chini kwenye uwanja
wa nyumba baada ya kurudi kukata bondeni, kwa ajili ya kutumia kwa kupikia.(PICHA NA ABDI SULEIMAN)
BAADHI ya kuni ambazo hutumika kwa ajili ya bekari
za mikate, zikiwa zimekusanywa nje ya bekari hiyo kwa ajili ya matumizi.(PICHA NA ABDI SULEIMAN)
BAADHI ya majiko sanifu yakiwa tayari
yameshatengenezwa kwa ajili ya kutumika majumbani, ambapo jiko moja huzwa kati ya
shilingi 5000.(PICHA NA ABDI SULEIMAN)
NA ABDI
SULEIMAN.
NI
MAJIRA ya saa 7:30 za mchana, nikiwa katika kijiji cha kambini Kichokochwe,
huku jua kikali kikiwaka mithili ya hakujanyesha mvua.
Hapa
nakutana Asha Omar Hamdan (46) mama wa watoto wanne, kwa sasa anatumia jiko
sanifu katika shughuli zake kupikia nyumbani, baada ya kupata maradhi katika
utumia jiko la mawe matatu.
“Hebu
tizama nilivyoathirika kutokana na jiko, hili la mawe matatu moto wake mkali
sana wakati unapipikia, macho yamepiga wekundu na mwili kazi kuwasha kila
wakati”alisema.
Asha
alisema hakua na lakufanya kwani hata wazazi wake wametumia jiko la mawe matatu
kupikia, lakini baada ya kuona hali kwake imekua ngumu, amelazimika kutafuta
jiko sanifu katika matumizi yake ya nyumbani.
Jiko sanifu
la kuni mbili ni katika majiko bora ya kupikia, jiko halitowi moshi wala moto
wake hauathiri mili kutokana na kutoka sehemu moja na sio kama jiko la mawe
matatu.
Amesema
uzuri wa jiko sanifu linatumia kuni kidogo, halichafuwi sufuria pia linaivisha
haraka chakula kama kuchemsha chai dakika nane (8) baada ya moto kushika, huku
jiko la mawe matatu ndani ya dakika 10.
Ali Khamis
Ahemde (56) ni mume wa biasha, anasema baada ya biasha kulalamika kwa muda
mrefu na kutumia dawa mbali mbali, kwa kutibu muwasho na kupona ndipo alipoamua
kutumia jiko sanifu katika matumizi yake ya kupikia.
Alisema
uwepo wa jiko hilo limeweza hata kumpunguzia mzigo mkubwa wa kwenda kutafuta
kunia, ndani ya mwezi mmoja alikuwa anakwenda mara mbili kutafuta kunia.
Ikumbukwe
kuwa kabla ya kuwepo kwa majiko sanifu, misitu ilikuwa katika hali mbaya sana,
kutokana na ukataji wa miti kwa ajili ya kuni za kupikia, ambapo zaidi ya
hekta 1000 zinapote kila mwaka, kwa mujibu wa mkuu wa Idara ya Misitu na
Mali zisizorejesheka Pemba Said Juma.
WANAOPIKIA MAJIKO SANIFU WANAYAPI WAO.
Fatma
Shaame Hamad mkaazi wa kambini Wilaya ya Wete, amesema majiko sanifu ni majiko
mazuri na rafiki mkubwa wa misitu, majiko haya hutumia kuni moja au mbili au
tatu katika matumizi yake ni tofauti na majiko ya mawe matatu ambayo yanatumia
kuni nyingi.
“Hebu
tizama hili jiko linavowaka hapa nimetia kuni 12, kila upande kuni nne kama
ingekuwa jiko sanifu jee, nimeshamaliza kupika dakika nane tu kama unachemsha
samaki, kuni chache tu na unamaliza haraka sana kupika”amesema”
Ashura Mzee
Haji mkazi wa kiungoni, miaka mitatu sasa bado anatumia jiko sanifu katika
shughuli zake za kupikia, huku akiwa na matumizi madogo ya kuni.
“Mimi
nimeshazowea kutumia majiko haya tena, yanaivishamara moja chakula, wala
halichafui sufuria kwa moshi kama majiko yale ya mawe matatu ambayo yanatumia
kuni nyingi” alisema Ashura.
Kuni
tunazoenda kutafuta kwa sasa zinatusaidia sana, kabla ya jiko hili sanifu kila
baada ya siku nne tukatafute kuni, sasa hivi tunafika wiki mbili hatuendi
kutafuta tena kunia.
Kombo
Khamis Ali mkaazi wa shengejuu, majiko sanifu yamempunguzia usumbufu wa kwenda
kutafuta kuni, muda mwingi sasa anafanya shughuli zake kutokana na jiko hilo
kutumia kuni kidogo.
“Ilikuwa
tunatumia zaid ya masaa mawili kwenda kutafuta kuni, kila wiki tunarudi tena
mbondeni kukata kuni, inafika wakati tunafukuzana na watu wa misitu, kama kuni
ndogo ndogo hakuna unakata japo mti mbichi unaenda kuuwandika ukikauka
unatumia”aliongeza.
WATENGENEZAJI
WA MAJIKO SANIFU WANASEMAJE
Salama
Khalfan Khamis mtengenezaji wa majiko sanifu kijiji cha Sahengejuu, alisema kwa
sasa soko la majiko yameshuka, kutokana na wananchi wengi kupata elimu ya
kutengeneza wenyewe.
Amesema
kuwa jiko hilo moja huuzwa kati ya shilingi shilingi elfu 5000, kwati haya ya
mawe matatu mtu hutengeneza tu, lakini jiko sanifu ni bora zaidi hata kupikia
kuliko la mawe matatu, sanifu sufuria linakaa bila ya hofu wakati hili jengine
mtumiaji anapawa kuliweka kwa uwangalifu sufuria.
Majiko
sanifu yanafaida nyingi, hutumia kuni kidogo, huhifadhi mazingira katika suala
la ukataji wa miti, gari moja ya Ng’ombe hupakia koroja tatu, koroja moja huwa
na vigogo 20, ambapo ukichanja kwa shoka korja moja kwa jiko sanifu unatumia
mwezi mmoja na nusu, kwa jiko la mawe matatu ni wiki tatu.
Mwajuma
Hamad Hamad anasema ugumu wa utengenezaji wa jiko hilo, ni upatikanaji wa udogo
tu, ambao hulazimika kuufata sehemu za mbali na hutumia gari za Ng’ombe katika
kubebea.
“Hili jiko
halina tabu sana katika utengenezaji panahitajika udongo, unaochanganywa na
maji, bati la kuwekewa kiwango cha jiko kulingana na bei dogo shilingi elfu
5000 na kubwa 8000, wala halitumii muda mrefu kutengeneza ikiwa mahitaji
yamekamilika ni dakika 10 hadi 15 kwa jiko moja, baadae linachomwa na moto ili
kuwa imara zaidi”amesema.
Kwa sasa
changamoto kubwa ni upatikanaji wa udongo tu, kwa sasa udongo waliokuwa
wakitumia umechanganyika na maji chumvi.
Katika
kukabiliana na ukataji wa miti, tumelazimika kupanda miti mingi ya jamii na
imekuwa misitu mzuri, yote ni kutokana na makubaliano kama tukiendelea
kuharibu misitu kwa ukataji wa kuni mwisho kutakua na jangwa.
VIONGOZI
WA ASASI ZA KIRAIA WANASEMAJE
Mkurugenzi
Mtendaji wa Community Forest Pemba, Mbarouk Mussa Omar amesema, sababu
iliyopelekea kuwa na mradi wa kutengeneza majiko sanifu na banifu, kutokana na
uharibifu wa mazingira, kwa upoteaji wa rasilimali ya misitu imekuwa ni kubwa.
Sababu
nyengine muda ni mkubwa ambao wanaoutumia akinamama, baba na vijana kwa ajili
ya kutafuta kuni na misitu ya asili imeshapotea, huku nguvu nyingi na muda
mkubwa unatumika katika utafutaji wa kuni.
Amesema
sabubu ya tatu ni misitu mingi ya asili Kisiwani Pemba, imeshapotea na haya
majiko ni marafiki mkubwa wa mazingira na misitu itaweza kurudi katika
haiba yake.
“majiko
sanifu yanatumia kuni chache, kwa mfano kuni mbili, tatu hata moja na unaweza
kupikia nyungu zako zote na moshi pia hautoki, tafauti na kutumia majiko ya
mafya matatu yanayotumia kuni nyingi”amesema.
“Majiko
haya pande zote unaweza kutia kuni na sio rafiki kimazingira, moshi mwingi
unatoka hupelekea kuathiri hata macho kutoka meupe na kuwa mekundu”ameongeza.
Tuliyalenga
maeneo 18 lakini baada ya kuonekana elimu inahitajika zaidi, juu ya matumizi ya
majiko sanifu tumefkia maeneo 36, sisi hatukurudi nyuma lengo letu kuyafanya
mazingira kuwa salama.
“Tuliweza
kutengeneza majiko sanifu 1738, katika utekelezaji wa mradi kuna maeneo tayari
wananchi wameenza kupanda miti ya matunda kuhifadhi uharibifu na kuepuka
mabadiliko tabia nchi”alifafanua Mbarouk.
Jumuiya
ya Sanaa, Elimu ya Ukimwi na Mazingira (JISEUMA) kisiwa Panza, imesema majiko
sanifu ni rafiki wa mazingira na yanasaidia kurudisha haiba ya misitu ambayo
imepotea kwa kiasi kikubwa.
“Miti mingi
imepotea huku kisiwani kwetu ilifika hadi makaburi yalifikwa na maji ya chumvi,
kutokana wananchi kukata miti ya mikoko kwa wingi kwa shuhuli za kijamii,
ikiwemo kupikia au kujengea n ahata kwa ajili ya mkaa”alisema.
Katibu wa
jumuiya hiyo Juma Ali Mati amesema wamelazimika kupanda miti zaidi ya
50000, katika maeneo mbali mbali ili kurudisha haiba ya asili ya kisiwa, sasa
wananchi wanatumia majiko hayo kwa shughuli zao za kupikia, licha yaw engine
bado kuendelea kutumia majiko ya mafia matatu.
Kwa mujibu
wa Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Dunia (SDGs) lengo namba 15, lnazungumzia
kulinda, kuanzisha na kuboresha matumizi endelevu ya mifumo ya ikolojia, kwa
kufanya menejiment ya misitu kukabili majanga.
“Hekta
Milioni 13 za misitu hutoweka kila mwaka, huku watu Milioni 1.6 hutegemea
misitu kwa maisha yao ikiwemo wenyeji wa misitu Milioni 70” kwa mujibu wa SDGs
lengo namba 15.
Kwa mujibu
wa hutuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Fedha za Wizara ya Kilimo
Maliasili na Uvuvu Zanzibar, mwaka wa fedha 2018/2029 Waziri Rasshidi Ali Juma,
alisema takwimu zinazonyeha ongezeko kubwa la matumizi ya nishati ya kuni,
kutoka mita za jazo 19,532,25 mwaka 2016, hadi kufikia mita za ujazo 23,114
mwaka 2017.
Hii
inatokana na wananchi wengi wa Unguja na Pemba kuelekeza nguvu zao katika
matumizi ya majiko ya mawe matatu, bekari za mikate kuendelea kutumia kuni.
VIONGOZI WA SERIKALI WANASEMAJE
JUU YA MAJIKO SANIFU
Mwalim
Khamis Mwalim, Mkuu wa Idara ya Mazingira Pemba, amesema matumizi ya majiko
sanifu yana umuhimu mkubwa hususan katika Kisiwa cha Pemba, imetokana na uwepo
wa ukataji wa miti hovyo, wakat kipindi cha nyuma sehemu nyingi miti
iliharibiwa kutokana na sababu ya upatikanaji wa nishati ya kupikia.
“Majiko
sanifu yanatumia kuni kidogo, miti mingene inabakia kwa kuendelea kuhifadhi
mazingira, kwa sasa hali ya kimazingira ilivyo, mwamko ni mkubwa wa upandaji wa
miti hususana miti ya kisasa, kama mivinje na miti ya asili inaendelea kupitia
vikundi vingi vya uhifadhi wa mzingira”amesema.
Moshi ni
mchanganyiko wa gesi mbali mbali mtu anapovuta moshi kwa muda mrefu, maradhi
mbali mbali ikiwemo muwasho, macho kuwa wekundu yote ni kutokana na utumiaji wa
majiko ya mawe matatu.
Wakati
umefika sasa kwa wananchi kutumia majiko sanifu, ili kupunguza matumizi ya muda
mrefu kwenda kutafuta kuni, ungeweza kufanya shuhuli nyengine, pamoja na
kulinda afya zao.
Mkuu wa
Idara ya Misiru na Malia Asili zisizorejesheka Pemba, Said Juma Said amesema
majiko sanifu yana umuhimu mkubwa sana kwa wananchi wa kisiwa cha Pemba, katika
suala la la uhifadhi wa mazingira inatokana na wananchi miaka mingi wakitumia
majiko ya mawe matatu
Majiko hayo
yanatumia kuni nyingi, hivyo ukataji wa misitu umekuwa ni mkubwa sana kwa kuni
za kupikia, kuwepo kwa majiko sanifu yamesaidia kuhifadhi mazingira kwa kutumia
kuni kidogo na kuwepo matumizi endelevu ya misitu.
“Majiko
haya yanasaidia uhifadhi wa misitu na kuwa endelevu kwa vizazi vilivyopo na
vijavyo”alisema.
Majiko
mkombozi ni miongoni mwa majiko sanifu, mkombozi zaidi yamejengwa kwenye
taasisi za ulinzi, pamoja na skuli zenye mabweni ya kulalia wanafunzi kutokana
taasisi hizo kutumia kuni kwa wingi, wakati jiko mkombozi hatumii kuni sana.
Mpaka sasa
kuna vijiji vimenufaika na majiko sanifu kama vile Makangale, Mjini Wingwi,
Tumbe, Wingwi Mtemani, Kiuyu kwa manda, Gando, Kambini, Kiungoni, Kengeja,
Wambaa, Makoongwe, ambapo zaidi ya majiko 200 yameshagawiwa katika vijiji hivyo.
Kwa mujibu
wa mkuu wa idara ya misitu na Malili zisizorejesheka Pemba, imesema zaidi ya
majiko sanifu 5000 watu wanatumia kwa sasa, baada ya kupatiwa elimu mbali mbali
juu ya matumizi ya majiko hayo, huku Mkoa wa Kaskazini Pemba ukiongoza kwa matumizi
ya majiko sanifu.
Kwa mujibu
wa utafiti wa Woody Biomass wa mwaka 2013, uliofanywa na Wizara ya Kilimo Mali
asili zanzibar, kupitia idara ya Misitu na Rasilimali, imesema eneo la
Zanzibar ni karibu 2 653 km 2 (Unguja 1 583 km 2 na Pemba 1 070 km 2 ).
Kwa mujibu
wa sensa ya watu na wenyeji wa Zanzibar ni 1 303 569 (sensa ya kitaifa 2012) na
kiwango cha ukuaji wa sensa ya wastani wa asilimia 2.8% ni saizi ya
familia ya watu 5 kwa mmoja, rasilimali za misitu inachukuwa jukumu
muhimu katika maisha ya kila siku ya watu kupata nishati kupikia, ujenzi wa
mbao, utalii, lishe, vyanzo vya maji, malazi ya wanyama wa porini na milango ya
maeneo ya ufugaji samaki.
“Mmahitaji misitu Zanzibar ni ya kisheria chini ya kifungu
cha 9 (1) cha Sheria ya Usimamizi na Uhifadhi wa Misitu no. 10 ya 1996. Msitu
wa Zanzibar”ulisema utafiti huo.
Kiasi cha kuni nchini Zanzibar kinaendelea kupungua wakati idadi
ya miti ikiongezeka, kiasi cha 8 633 290 m3 (mita qub) wakati
Unguja ni 5 523 536 m3 na kwa Pemba ni 3 109 754 m3
kwa mwaka 1997, wakati mwaka 2013 Unguja kulikuwa 5 782 500 m3
na Pemba ilikuwa 4 488 300 m3 .
Mratib wa kitengo cha elimu ya afya Pemba Dr Hamad Hamad Simba
asema kuwa moja ya kemikali hatari iliyomo ndani ya moshi ni carbonda oxaid,
nchi za Ulaya hutumika sana kama sumu ikiambatana na kemikali nyingine.
Amesema unapowasha moto wa kuni pele moshi unapotoka ule wa kwanza
wenyewe vipande vidogo vidogo vinavyopaa angani, vinaathari kubwa ndani ya
mwili unapovuta hewa hewa unaweza kupata magonjwa mbali mbali ikiwemo muwasho
machoni, maradhi ya moyo, kutiririka mafua, kifua na kiharusi.
Alisema
wataalamu wanatafautiana lakini wapo wanaosema karibu watu elfu 30,000,
hufariki duniani kila mwaka kutokana na moshi wa jikoni, huku waathirika zaidi
ni mama wajawazito, watoto wadogo, watoto wachanga na wazee.
HITIMISHO.
Sasa wakati
umefika kwa jamii kujikita zaid katika matumizi ya majiko sanifu yanayotumia
kuni chake chake za kupikia, kwa mautumia ya majumbani pamoja na bekari za
mikate kutumia nishati mbala ikiwemo nishati ya umeme, ili kupunguza wimbi
kubwa la ukataji wa miti kwa ajili ya matumizi ya kuni, taasisi na idara husika
wakati umefika kuendelea kuelimisha jamii na viongozi wa bekari za mikate, kila
kukicha miti inapotea itafika wakati Kisiwa cha pemba kitakuwa ni jangwa kwa
ukataji wa miti kwa ajili ya kuni.
EMAIL:abdi
suleiman33@gmail.com
No comments:
Post a Comment