Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na
Uokoaji (CGF) John Masunga (Kulia), akisalimiana na Kamishna wa Kikosi cha Zimamoto
na Uokozi Zanzibar, Ali Malimussy (kushoto), baada ya kuwasili Makao Makuu ya
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji jijini Dodoma.
Wakuu wa Vikosi vya Serikali ya Mapinduzi
Zanzibar (SMZ), wakiongozwa na Kamishna wa Kikosi cha Zimamoto na Uokozi
Zanzibar, Ali Malimussy watembelea Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na
Uokoaji nchini yaliyopo jijini Dodoma.
Lengo ni kukuza
mahusiano na ushirikiano kati ya vyombo hivyo.
Katika ziara hiyo Kamishna Jenerali wa
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CGF) John Masunga, alitumia fursa hiyo kuwapongeza
Wakuu wa Vikosi
hivyo kwa kazi
nzuri wanazozifanya na kuwaahidi ushirikiano katika kulijenga Taifa.
Aidha Kamishna Malimussy amemshukuru CGF John Masunga kwa niaba ya Ujumbe uliotembelea Makao Makuu
ya Jeshi hilo. “Tumejifunza
mengi lakini pia tunashukuru kwa kupata fursa ya kutembelea na kuona jinsi gani
tunaweza kushirikiana” alisema Kamishna Malimussy.
Kamishna wa Kikosi cha Zimamoto na Uokozi
Zanzibar Ali Malimussy, akisaini kitabu cha wageni wakati walipotembelea Makao
Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji jijini Dodoma, akiwa ameambatana na Wakuu
wa Vikosi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), lengo ni kukuza mahusiano
na ushirikiano kati ya vyombo hivyo, (Kulia) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la
Zimamoto na Uokoaji (CGF) John Masunga.
Kamishna wa Kikosi cha Zimamoto na Uokozi
Zanzibar Ali Malimussy, akifafanua jambo, wakati walipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
jijini Dodoma akiwa ameambatana na Wakuu wa Vikosi vya Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar (SMZ) mapema leo.
Kamishna wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar Ali Ali
(kulia), akimshukuru Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CGF)
John Masunga kwa niaba ya Ujumbe uliotembelea Makao Makuu ya Jeshi hilo
yaliyopo jijini Dodoma mapema leo.
Kamishna
Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CGF) John Masunga (katikati)
akiwa kwenye picha ya pamoja na Kamishna wa Kikosi cha Zimamoto na Uokozi Zanzibar, Ali Malimussy
(Wanne kutoka kushoto), Kamishna wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar Ali Ali (Watatu
kutoka kushoto), Mkuu wa Kikosi cha Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU) Ali hamad ( Wasita kutoka kulia), Wajumbe toka Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na Viongozi Waandamizi wa Jeshi
hilo wakati walipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji jijini
Dodoma mapema leo.
(PICHA NA JESHI LA
ZIMAMOTO NA UOKOAJI)
No comments:
Post a Comment