MJUMBE
wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM ) Taifa na Waziri Mkuu, Kassim
Majaliwa amewasihi wananchi wa Jimbo la Ruangwa kumpigia kura Rais Dkt.
John Pombe Magulfuli ili aendelee kujenga na kuimarisha huduma mbalimbali za
jamii nchini.
Akizungumza
wakati alipozindua kampeni za CCM katika jimbo la Ruangwa kwenye kijiji cha
Chinongwe leo Septemba 11, 2020, Mheshimiwa Majaliwa amesema maendeleo
makubwa yaliyofanyika nchini katika kipindi cha kwanza cha utawala wa Rais Dtk.
Magufuli kwa kiwango kikubwa yamebuniwa na kusimmiwa kwa karibu na Rais
mwenyewe.
Amesema
kwa kuwa bado ipo miradi mingi mikubwa iliyoanzishwa na Rais Dkt.
Magufuli inayohitaji kukamilishwa ni vyema Watanzania
wakampigia kura za kishindo zitakazompa nafasi ya kuliongoza Taifa kwa kipindi
cha pili ili aweze kumalizia miradi hiyo na kuanzisha mingine mingi kama
ilivyoonyeshwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020-2025.
Aliitaja
miradi inayotekelezwa ni ya ujenzi wa Bwawa la kufua Umeme wa maji la
Nyerere, Reli ya Kiwango vya Kimataifa ya SGR, ujenzi na uboreshaji wa
huduma za afya kama vile ujenzi wa Vituo vya afya, Hospitali za wilaya, Mikoa
na Rufaa pamoja na ujenzi wa miradi ya maji kuwa ni baadhi ya miradi
ambayo inamfanya Rais Magufuli astahili kupewa kipindi kingine cha
kuiongoza nchi.
Akizungumzia
mipango ya serikali ya kuongeza ajira kwa Watanzania, Mheshimiwa Majaliwa
amesema msukumo mkubwa uliofanywa na serikali ya Awamu ya Tano katika
kuhamasisha wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kujenga viwanda vidodo,
vya kati na vikubwa ni moja ya mikakati ya makusudi ya kuongeza ajira kwa
Watanzania.
“Kiwanda
cha samani na kiwanda cha kubangua korosho vinavyojengwa katika kijiji cha
Namkonjera wilayani Ruangwa ni moja ya juhudi zinazolenga kuwapatia
ajira wananchi wa wilaya hii na Watanzania kwa ujumla”
Kuhusu
Vitambulisho vya Wajasiriamali nchini, Mheshimiwa Majaliwa
amevitaja kuwa chanzo kingine cha ajira hasa kwa vijana ambao hapo awali
walibugudhiwa kwa kuonekana kuwa hawana uhalali wa kufanya biashara katika
baadhi ya maeneo hasa ya katikati ya miji na majiji .
Mheshimiwa
Majaliwa amesema bugudha kwa vijana hao hivi sasa imekwisha na sasa
wanafanya biashara zao ambazo ni ajira halali inayotambuliwa na
Serikali ambayo inayowapa kipato cha kuendesha maisha yao na familia zao
.
Katika
hatua nyingine Mheshimiwa Majaliwa aliwashukuru wanaRuangwa wananchama wa vyama
vyote vya siasa kwa kumpitisha bila kupingwa katika jimbo hilo.
Naye
mgombea ubungea wa Jimbo la Ndanda, Cecil Mwambe alipopewa nafasai ya
kuzungumza amesema Ilani ya Uchanguzi ya CCM ya 2020-2025 imegusa maisha
ya wananchi wa Ruangwa kwani imezungumzia maboresho ya zao la
korosho pamoja masoko yake.
Mheshimiwa
Mwambe amewaomba wanaRuangwa wamchague Rais Dkt. Magufuli na Madiwani wa
CCM kwani Ilani ya CCM imezingatia maslahi yao hasa kilicho cha mazao ya
Biashara na chakula.
Mbuge
Mstaafu wa Viti Maalum, Riziki Lulida aliyerejea CCM akutoka Chama cha
CUF aliwaomba wanaRuangwa kumuunga mkono Rais Dkt. Magufuli kwa
kumpa kura nyingi kwani kawafanyia mengi na makubwa wana Lindi
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, SEPTEMBA 11, 2020.
No comments:
Post a Comment