Baadhi ya Vijana wenye vipaji katika Sanaa ya
Muziki wanaolelewa na kituo cha Tanzania House of Talents (THT) na viongozi wa
kituo hicho wakiwa katika picha ya pamoja na
na Katibu Mkuu Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi
aliyeketi (watatu kushoto) leo Desemba 04, 2020 Jijini Dar es Salaam,
alipotembelea kituo hicho kwa lengo la kuona namna kinafanya kazi na kuahidi
kuwa mlezi wao.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt.Hassan Abbasi ameielekeza Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo kuanza kushirikiana na Tanzania House of Talents (THT) katika mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wa Muziki.
Dkt. Abbasi ametoa kauli hiyo leo Desemba 04, 2020 alipotembelea kituo hicho kilichopo Jijini Dar es Salaam, kuangalia maendeleo ya vijana wanaolelewa na kituo hicho kilichokuwa kimeanzishwa na marehemu Ruge Mutahaba kwa lengo la kukuza vipaji vya sanaa ya muziki kwa vijana na kuwajengea uwezo wa kujiendeleza .
Akizungumza
katika ziara hiyo Dkt.Abbasi alisema wizara inatambua mchango wa THT katika
kukuza tasnia ya muziki na inaheshimu vipaji vya vijana wanaolelewa na taasisi
hiyo, pia inafahamu maono ya mwanzilishi wake kuhusu kuendeleza kituo hicho na
ipo tayari kuwapa ushirikiano.
“Nitaunganisha
wadau wote wenye nia na mapenzi mema ya kukuza Sanaa na kuendeleza kituo hichi, nikiwemo mimi
mwenyewe ili tuwe walezi wa THT kwa kipindi chote,” alisema Dkt.Abbasi.
Pamoja
na hayo nae Msimamizi wa Kituo hicho kwa sasa Kemmy Mutahaba alieleza kuwa THT
imekuwa ikifanya kazi kwa takribani miaka 15 sasa, na kazi yake kubwa ni kuibua
na kukuza vipaji vya vijana katika
tasnia ya Muziki ili waweze kujikwamua kiuchumi.
“THT
imekuwa ikilea vijana katika misingi ya uzalendo kwa kusimamia msemo huu wa marehemu Ruge kuwa Watu
wenye njaa ya mafanikio hawatazami ukubwa wa changamoto, wanatazama ukubwa wa
ndoto,” alisema Kemmy.
Halikadhalika
nae mama Mzazi wa Marehemu Ruge Christina Mutahaba ambaye ndiyo mwanzilishi wa
kituo hicho alitoa ombi kwa serikali kuendelea kutoa ushirikiano wa kuendeleza
kituo hicho cha THT ili kuendelea kuishi ndoto za mwazilishi wake..
Akihitimisha
ziara hiyo Dkt. Abbasi alisema kuwa serikali itaendelea kushirikiana na kituo
hicho , pia alitembelea studio ya kituo
hicho na kuahidi kutafuta wadau watakaosaidia upatikanaji wa vifaa ambavyo ni
vibovu, pia aliwasihi kushiriki katika Tamasha la Serengeti Music and Arts
Festival linaloandaliwa na serikali na litafanyika Desemba 26,2020.
No comments:
Post a Comment