Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Omar Hassan King akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu Michuano ya Mapinduzi Cup hafla iliyofanyika Ukumbi wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale.
Na Rahima Mohamed / Mariam Kidiko - Maelezo
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Omar Hassan King amewataka wananchi kushiriki katika michuano ya Mapinduzi Cup kwa lengo la kuleta umoja na kuimarisha sekta ya michezo nchini.
Hayo ameyasema katika ukumbi wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Kikwajuni Mjini Unguja wakati akizungumza na waandishi wa habari amesema mashindano hayo yanatarajiwa kuwa na makundi manne makubwa ambayo yataandaliwa kitaifa.
Alisema makundi hayo ni kama vile Mapinduzi Cup ya wakubwa, mashindano yatakayoshirikisha Wizara na taasisi za Serikali ya Zanzibar na Tanzania zilizopo Zanzibar , ZBC Mapinduzi Cup watoto pamoja na Mapinduzi Cup ya timu za wanawake.
Alifafanua kuwa Mapinduzi Cup wakubwa yatashirikisha timu za Zanzibar na Tanzania Bara ambapo timu tisa zitashiriki katika mashindano ikiwemo timu ya Simba, Yanga, Mlandege, Mtibwa Sugar, Malindi, Jamuhuri,
Alisema kwa upande wa mashindano yanayoshirikisha Wizara,Taasisi na mashirika ya Serikali ya Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ofisi zake zipo Zanzibar.
Vilevile alisema mashindano ya ZBC Mapinduzi Cup watoto yatashirikisha vijana wenye umri mdogo kutoka Wilaya kumi na moja za Zanzibar kwa lengo la kuibua vipaji .
Hata hivyo alisema kwa mwaka huu wanategemea kuwa na mashindano ya Mapinduzi Cup ambayo yatashirikisha timu za wanawake na yaataandaliwa na Shirikisho la soka Zanzibar .
Michuano hiyo yanatarajiwa kuanza mwanzoni mwa mwezi ujao kwa kutegemea ratiba ya ligi za Tanzania Bara sambamba na kuunda kamati maalum kwa ajili ya kuratibu mashindano hayo.
No comments:
Post a Comment