Habari za Punde

TAMWA Zanzibar yasikitishwa na hukumu ya kumuachia huru mtuhumiwa aliyembaka mtoto wake wa kumzaa

Na Mwandishi wetu 

Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA, ZNZ) hakikuridhishwa  na  hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Wete Mkoa wa kaskazini Pemba kumuachia huru  mtuhumiwa aliyembaka mtoto wake wa kumzaa.

TAMWA imepokea taaarifa za Salim Khamis Ali mwenye umri wa miaka (43) mkaazi wa Taifu shehia ya Kinyasini, kisiwani Pemba aliyembaka mtoto wake wa kumzaa huko Pemba ameachiwa huru kwa madai kuwa  taarifa za daktari zimeonesha kwamba mtoto huyo ni mzoefu kwa maana ya kuwa ameshatenda tendo la ngono hapo awali.

Tukio hilo liliripotiwa katika kituo cha polisi Wete tarehe Desemba 6/ 2019 na kufunguliwa jalada namba IR471/2019 ambapo jalada hilo lilieleza kwamba Salim Khamis Ali anatuhumiwa kumbaka mtoto wake wakike aliye chini ya umri wa miaka 13.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.