Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano
na Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu akipata maelezo juu ya Ujenzi wa Bwalo la Mitihani
kwa wanafunzi (halipo pichani) kutoka kwa Mkurugenzi wa Uratibu shughuli za
Serikali – SMZ Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Bw. Khalid Khalid Hamrani Mkurugenzi,
hii leo Fujoni Zanzibar.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano
na Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na wananchi na wafanya biashara katika soko la Kinyasini ikiwa
ni moja miradi ya Muungano inayotekelezwa pande zote. Waziri Ummy ametoa rai
kwako kujuvunia matunda ya Muungano.
Na Lulu Mussa
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu amesema
watanzania wote wanao wajibu wa kujivunia matunda ya Muungano ikiwa ni pamoja
na miradi ya Maendeleo inayotekekezwa pande zote mbili za Muungano.
Akiwa
visiwani Zanzibar katika siku yake ya pili ya ziara ya kikazi, Waziri Ummy
ametembelea miradi ya TASAF na MIVARF ikiwa ni pamoja na Kituo cha Afya Kianga,
Bwalo la Wanafunzi na Soko la Mbogamboga la Kinyasini.
Amesema pamoja na changamoto zilizopo zipo
fursa kwa Watanzania kujiletea maendeleo na ustawi wao, kwa kuwa kuwepo kwa
fursa hizo kumeleta tashwishi na matarajio makubwa kwa wananchi katika
kuendeleza mafanikio yaliyopatikana na kuchochea mafanikio katika maeneo
mengine kwa maslahi ya Taifa
“Tumejionea wenyewe mpango huu mkubwa wa
kunusuru kaya maskini kupitia Muungano wetu
unatekelezwa na pande zote mbili na haya ndio matunda ya Muungano kuhakikisha
miradi mikubwa inatekelezwa pande zote mbili” Ummy alisisitiza.
Aimetaja baadhi ya Miradi ya maendeleo inayotekelezwa
na Serikali zeto mbili yenye kunufaisha
wananchi wake iko katika Nyanja za Elimu; Afya; Masoko; Maji; Mazingira pamoja na
Usafiri na Usafirishaji.
“Kama mnavyofahamu tunataka kuulinda, kudumisha na kuuimarisha
muungano wetu kwani ndio umoja wa
watanzania, ndio usalama wa watanzania na ndio amani ya watanzania wote” Alisisitiza
Mhe. Waziri
Kupitia mradi wa MIVARF takriban masoko 16 yamejengwa Tanzania nzima
kati ya hayo masoko 4 yamejengwa Zanzibar, kituo cha afya Kianga chenye kunufaisha
takriban Shehia 3 za Kianga, Dole na Mazizini huku kikihudumia takribani wakazi 19,840,
ujenzi wa madarasa katika Skuli za Fujoni na Mahonda ambazo zimeweza kutatua
changamoto za elimu.
Waziri
Ummy Mwalimu amesema kuwa ni vyema tukatumia ipasavyo fursa zilizopo Tanzania
Bara na Zanzibar kwa kuleta maendeleo yatakayoinua hali ya uchumi wa Watanzania,
na kutoa rai ya kuulinda, kuuimarisha na kuudumisha Muungano wetu kwani ni dira
ya mafanikio yetu.
Kwa upande
wake Mjumbe wa Baraza la Uwakilishi (Mwera) Mhe. Mihayo Juma N’hunga ameshukuru
Serikali kwa kupata kusogeza huduma zenye kugusa Maisha ya wananchi.
No comments:
Post a Comment