Na. Beatrice Sanga-MAELEZO
Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) inatarajia kufanya maonesho ya Kimataifa ya Utalii ( Swahili International Tourism Expo ) maarufu kama “SITE” yatakayoanza Oktoba 8 hadi 10, 2021 Mlimani City Jijini Dar es Salaam na kushirikisha Mawakala wa Utalii wa Kimataifa, waandishi wa habari za utalii wa Kimataifa, na wafanyabiashara wa utalii kutoka Tanzania na nchi za jirani
Akizungumza
na waandishi wa habari Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania Bi Devota Mdachi,
amesema Bodi kwa kushirikiana na Balozi za Tanzania ng’ambo imejipanga kuwavutia mawakala wa utalii na waandishi wa
habari za utalii wa Kimataifa kutoka nchi zao za uwakilishi pia kuvutia
makampuni ya uoneshaji yapatayo 200 kutoka Tanzania, Nchi za Afrika Mashariki,
Kati, Kusini na Afrika Magharibi
“Kama
kawaida yetu, onesho litakuwa na programu
kadhaa zitakazo ongeza mvuto kwa
mawakala wa kimataifa wa utalii, lakini pia tumejipanga kuendesha programu ya
ziara ya mafunzo kwa baadhi ya mawakala
wa utalii na waandishi wa habari za utalii wa Kimataifa , onesho litakuwa na programu za semina mbalimbali
ambazo pamoja na masuala mengine zitalenga
kutoa elimu kwa washiriki kuhusu mikakati ya kuvutia watalii katika
kipindi hiki cha Janga la Corona”, amesema Mdachi
Aliongeza
kuwa, SITE ya mwaka huu inabeba umuhimu
mkubwa na wa kipekee kwa mawakala wote wa utalii wa Tanzania kwa kuzingatia
kuwa fursa za maonesho ya Kimataifa kama hayo bado hazijafunguka katika nchi
nyingine kwa sababu ya changamoto ya ugonjwa wa Corona.
Amebainisha
kuwa, TTB ina uhakika wa kuwapata mawakala
wa kimataifa, kutokana na makundi ya mawakala na watalii ambao imekuwa
ikiwaleta baada ya Tanzania kufungua anga ambapo mpaka sasa Tanzania imeweza
kupokea mawakala na watalii kutoka Nchi
mbalimbali kama Urusi, Ukraine, Poland, Czech, Japani, Uhispania, Ufaransa,
Uturuki na Uingereza .
Naye,
Kaimu Meneja wa Masoko ya Ndani, Joseph Sengwa, ametoa wito kwa wadhamini,
wadau, na wananchi kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kutembelea onesho hilo ikiwa
ni sehemu ya utalii wa ndani na kupata elimu kuhusu biashara za utalii lakini pia makampuni ya biashara za hoteli na mawakala wa
utalii kuweza kutumia fursa
zinazopatikana katika onesho hilo kwa ajili ya kujitambulisha na kujitangaza zaidi katika sekta ya utalii
“Makampuni
yenye uwezo wa kudhamini onyesho hili napenda kuwahakikishia kuwa udhamini wao
kwa onesho la SITE ni fursa ya kipekee kujitambulisha kwenye sekta ya utalii
ambayo inamatumaini makubwa kushamiri kwa kasi (To bounce back) mara dunia
itakapofunguka. Amesema Sengwa
No comments:
Post a Comment