TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR
TAARIFA
YA TUME YA UCHAGUZI KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU UTARATIBU WA UENDESHAJI WA
KAMPENI ZA UCHAGUZI MDOGO WA JIMBO LA PANDANI NA WADI YA KINUNI KATIKA KIPINDI
CHA MAOMBOLEZO YA KIFO CHA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Ndugu Waandishi wa Habari,
Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ZEC inaendelea na maandalizi ya Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Pandani na Wadi ya
Kinuni unaotarajiwa kufanyika tarehe 28 Machi 2021, kutokana na aliyekuwa
Mwakilishi Mteule wa Jimbo la Pandani na Diwani Mteule wa Wadi ya Kinuni
Kufariki Dunia mwezi wa Novemba, 2020. Wakati Tume ikiendelea na maandalizi
hayo Usiku wa jana tarehe 17/03/2021
tumepokea taarifa ya kifo cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Joseph Pombe Magufuli. Mungu ailaze roho ya Marehemu mahala pema peponi.
(Amiin).
Kutokana na msiba huu,
Serikali imetangaza siku 14 za maombolezo ya kitaifa. Kwakuwa kampeni za vyama
vya Siasa kwa ajili ya Uchaguzi Mdogo huo zinaendelea katika maeneo mbali mbali
ya Jimbo la Pandani na Wadi ya Kinuni, Tume ya Uchaguzi kwa Mamlaka iliyonayo
inatangaza utaratibu mpya wa kuendesha kampeni katika kipindi hicho cha
Maombolezo kama ifuatavyo:-
i.
Viongozi wa vyama vya siasa
na Wagombea ambao wanaendelea na Kampeni zao waache kupiga Muziki, kuimba nyimbo
za Kisiasa na wasitishe shamrashamra za sherehe wakati wote wa kipindi cha
Maombolezo.
ii.
Viongozi wa vyama vya siasa
na Wagombea wawatake wafuasi wao kabla ya kuanza mikutano ya hadhara kutenga muda
angalau wa dakika moja kusimama na kukaa kimya na kumuombea dua Marehemu.
iii.
Viongozi wa vyama vya siasa
na Wagombea wanatakiwa kuacha kufanya kampeni siku ya mazishi.
iv.
Viongozi wa vyama vya siasa
na Wagombea wanasisitizwa kutumia matumizi ya maneno mazuri na lugha inayoendana
na wakati huu wa maombolezi.
Ndugu Waandishi wa Habari, Tume
ya Uchaguzi inasisitiza kuwa, tarehe ya Uchaguzi Mdogo iko kama ilivyopangwa na
inawataka Wagombea wa Uchaguzi Mdogo
kuendelea na kampeni zao huku ikisisistiza kuelewa kua Taifa lipo katika Kipindi cha maombolezo juu
ya Msiba wa Kiongozi Mkuu wa Taifa la Tanzania.
Tume ya Uchaguzi ya
Zanzibar inatumia nafasi hii kumuombea Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli
apumzike kwa amani na kuwaombea Watanzania
kuwa na subira wakati wote wa Msiba.
MUNGU
IBARIKI ZANZIBAR
MUNGU
IBARIKI TANZANIA
Ahsante Sana
JAJI
MKUU (Mst) HAMID MAHMOUD HAMID
MWENYEKITI
TUME
YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR
ZANZIBAR
18
MACHI,2021
No comments:
Post a Comment