Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Faustine Ndugulile (mwenye
suti ya kijivu) alipowasili uwanja wa ndege wa Pemba kwa ajili ya kuanza ziara
ya kutembelea vituo vya TEHAMA vilivyojengwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote
(UCSAF) kisiwani hapo. Kushoto kwake ni Waziri Kindamba Mtendaji Mkuu wa
Shirika la Mawasiliano Tanzania
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Faustine Ndugulile (mwenye
suti ya kijivu) akisalimiana na baadhi ya watendaji wa Wizara hiyo pamoja na
Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
kabla ya kuanza ziara ya kutembelea vituo vya TEHAMA kisiwani Pemba. Kushoto
kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
Dkt.Zainab Chaula
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Faustine Ndugulile (mwenye
suti ya kijivu) akizungumza na watendaji
wa Wizara hiyo pamoja na Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi ya Serikali
ya Mapinduzi Zanzibar kabla ya kuanza ziara ya kutembelea vituo vya TEHAMA
kisiwani Pemba. Kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na
Teknolojia ya Habari Dkt.Zainab Chaula
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari,
Dkt. Faustine Ndugulile wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (katikati)
akipokea maelezo kutoka kwa mdhamini wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na
Uchukuzi ya Serikali ya Mapinduzi kisiwani Pemba Ibrahim Juma (kushoto) katika
kituo cha TEHAMA cha Micheweni TEHAMA kisiwani Pemba. Kulia ni Katibu Mkuu wa
Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt.Zainab Chaula
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Faustine Ndugulile (kwa tatu kushoto)
akizungumza katika kituo cha TEHAMA cha Wete kisiwani Pemba. Kutoka kushoto ni
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Amour Bakari,
akifuatiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Wizara hiyo Dkt. Mzee Mndewa na
Kulia ni Waziri Kindamba Mtendaji Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Faustine Ndugulile (Katikati) akitoka kukitembelea kituo cha TEHAMA cha Micheweni kisiwani Pemba akiambatana na baadhi ya watendaji wa Wizara hiyo pamoja na na Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
Na Faraja
Mpina- WMTH, Zanzibar
Waziri wa
Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile amefanya ziara
ya kutembelea vituo vya TEHAMA Kisiwani Pemba vilivyopo Wete, machomane,
Micheweni na Chonza ambavyo ni miongoni mwa vituo kumi vilivyojengwa na Mfuko
wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kwa gharama ya shilingi 1,138,000,000 visiwani
Zanzibar kwa ajili ya kutoa huduma za TEHAMA kwa wananchi.
Dkt. Ndugulile
amesema kuwa katika Wizara yake kuna maeneo ambayo ni ya kimuungano hivyo,
ziara yake ni kwa ajili ya kutembelea na kufahamu shughuli mbalimbali
zinazoendelea kufanyika ambazo ni za muungano na mojawapo ni vituo hivyo
vilivyojengwa na UCSAF, vinne kisiwani pemba na sita kisiwani Unguja ambapo
jumla ni vituo kumi.
“Tumeviona
vituo vya TEHAMA, vina kompyuta lakini havifanyi kazi, niziombe taasisi zangu
ziwe zinazungumza katika juhudi zetu tunazozifanya kwasababu tuna uwezo wa kushirikiana
kufanya kwa pamoja katika baadhi ya maeneo, sio mfano UCSAF anajenga jengo na
kuweka vifaa halafu halina intaneti wakati Shirika la Mawasiliano Tanzania
(TTCL) lipo lingeweza kuhakikisha intaneti inapatikana”, Dkt. Ndugulile
Aidha,
amezisisitiza taasisi za mawasiliano
kuangalia huduma zinazoweza kuwekwa katika vituo hivyo ili viweze kutoa huduma
ya pamoja na kusaidia uendeshaji wa vituo hivyo kuliko kuiachia mzigo Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar kuviendesha kwa kulipia gharama mbalimbali za
uendeshaji.
“Tukiweza
kufanya vizuri katika vituo vya TEHAMA vilivyopo, vitatupa nguvu zaidi ya
kupanua wigo wa vituo kama hivi katika maeneo mengine, ili huduma za TEHAMA
ambayo ni haki ya msingi ya kila mwananchi ipatikane kwa wigo mpana zaidi
visiwani hapa”, Dkt Ndugulile
Hata hivyo,
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Amour Bakari amesema
kuwa kutakuwa na mpango wa dharura wa kuhakikisha vituo hivyo vinaanza kufanya
kazi ndani ya muda wa wiki moja na baadae kutakuwa na mpango endelevu kwa
kuhakikisha vituo hivyo vinaendelea kutumika.
Aliongeza kuwa
wamefanya mazungumzo na TTCL ikiwa ni pamoja na taratibu za kufanya malipo ili
kuhakikisha Shirika hilo linafikisha
huduma ya intaneti katika vituo hivyo ili wananchi waanze kuvitumia.
Naye Katibu
Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania amesema kuwa Wizara hiyo ni ya muungano na wamekuja katika
vikao wa mashirikiano baina ya Wizara hizo mbili ili kuangalia mafanikio na
changamoto ili kuweza kuzitatua kwa pamoja.
“Katika ziara
hii nimekuja na watendaji wa Wizara na wa taasisi zetu zote za mawasiliano ili
kutembea pamoja kwa kila mmoja kujifunza kwa mwenzake na kutoka na mpango
mkakati wa kuhakikisha tunatatua changamoto zilizopo na kuzidi kuuimarisha
muungano wetu”, Dkt. Chaula
Naye Mkuu wa
Wilaya ya Mkoani kisiwani Pemba amesema kuwa amefarijika kuona Waziri huyo wa
Serikali ya Muungano ametembelea vituo hivyo na kudhihirisha Tanzania Bara na
Visiwani ni wamoja na yanayofanyika ambayo yanahusiana na sekta za muungano
yanatekelezeka katika pande zote mbili.
“Ziara hii
inadhihirisha tuna muungano imara na upo vizuri kufuatilia yale ambayo ni ya
pamoja ili kuweza kuhakikisha mapungufu yanafanyiwa kazi kwa kushirikiana na
kuyaweka vizuri, ndio maana ujio huu umetaja mpaka muda ambao vituo hivi
vitaanza kufanya kazi”, alisema
Imetolewa na
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya
Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
No comments:
Post a Comment