Habari za Punde

COSOTA Yakamata Wazalishaji 11 wa Kazi za Muziki na Filamu Bila ya Kuwa na Vibali vya Wamiliki -- KARIAKOO

Mwanasheria wa Taasisi ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA) Lupakisyo Mwambinga akifanya ukaguzi wa kazi zinzazozalishwa na moja ya Ofisi za Kariakoo iliyopo Mtaa wa Aggrey  uzalishaji wa kazi za Muziki na Filamu na kuwakuta  wakidurufu za Muziki wa Bongo Fleva na Filamu za nje bila ya kuwa mikataba au makubaliano ya wamiliki wa kazi hizo, Operesheni hiyo ya ukaguzi imefanyika mei 18,2021 Jijini Dar es Salaam. 

Mtuhumiwa wa Uzalishaji na Udurufu wa Kazi za Muziki na Filamu bila ya kuwa na kibali cha mmiliki wa kazi aliyekutwa akidurufu collection ya nyimbo za Muziki wa Bongo Fleva katika Ofisi yake iliyopo Kariakoo Mtaa wa Aggrey Bw.Ramadhan Sadiq akihojiwa na waandishi wa habari (hawapo pichani) mara baada ya kukamatwa katika Operesheni ya Ukaguzi wa Hakimiliki iliyofanywa na COSOTA Mei 18, 2021, Kariakoo Jijini Dar es Salaam.

Mtuhumiwa wa Uzalishaji na Udurufu wa Kazi za Muziki na Filamu bila ya kuwa na kibali cha mmiliki wa kazi aliyekutwa akidurufu Filamu za Nje ya nchi katika Ofisi yake iliyopo Kariakoo Bw.Frank Manyama ambaye ni Msimamizi wa Sanyiwa Production  akihojiwa na waandishi wa habari (hawapo pichani) mara baada ya kukamatwa katika Operesheni ya Ukaguzi wa Hakimiliki iliyofanywa na COSOTA Mei 18, 2021, Kariakoo Jijini Dar es Salaam.

 

Na Anitha Jonas – COSOTA,Dar es Salaam.19/05/2021

Taasisi ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA) imefanya operesheni katika baadhi ya maeneo ya uzalishaji wa kazi za Filamu na Muziki na ambapo kukamata zaidi ya mashine 50 zenye uwezo wa kudurufu takribani nakala 10,000 kwa nusu saa.

Operesheni hiyo ya uharamia wa kazi za Muziki na Filamu imefanyika Mei 18, 2021 Kariakoo, Jijini Dar es Salaam ambapo  takribani watuhumiwa kumi na moja wanafanya shughuli za uazalishaji wa kazi haramu za filamu na Muziki walikamatwa na kufikishwa Kituo cha Polisi Msimbazi kwa ajili ya kufunguliwa mashtaka.

Akizungumza katika Operesheni hiyo Mwanasheria wa COSOTA Bw.Lupakisyo Mwambinga alieleza kuwa suala uharamia wa kazi za Muziki na Filamu umekithiri nchini hivyo COSOTA imedhamiria kukomesha hilo kwa kufanya operesheni endelevu za kukamata kazi zote nje na ndani ambazo zinazalishwa bila kufuata sheria.

"Kifungu cha 42 cha Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki kamakilivyofanyiwa marekebisho na Sheria namba 3 ya mwaka 2019 kinasema ukikamatwa kwa kosa la uvunjifu wa Hakimiliki  faini yake ni isiyopungua milioni ishirini au Kifungo cha Miezi sita na kisichozidi Miaka Mitatu au vyote kwa pamoja,"alisema Bw.Mwambinga.

Pamoja hayo Mwanasheria huyo alitoa onyo kali kwa wazalishaji wote na wasambazaji wa kazi za Muziki na Filamu ambao wanaburn CD za Muziki na Filamu, wanaoweka Muziki kwenye flash kwa kusema kuwa hilo ni kosa, na alisisitiza kuwa COSOTA imedhamiria  tutahakikisha tunathibiti hilo na kwa yoyote atakayekamatwa na kazi hizo zisizo na mikataba au makubaliano na wamiliki atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Halikadhalika Bw.Mwambinga alifafanua kuhusu  udurufu wa Filamu za nje bila kufuata utaratibu kuwa ni kosa  na aliwasihi wazalishaji hao  kuachakudanganyana, kwa kusema udurufu au uzalishaji wa kazi za  nje bila kibali cha mmiliki unaruhusiwa,hivyo alisisitiza katika uuzalisha au udurufu wa kazi yoyote iwe Muziki au Filamu ya ndani au ya nje ya nchi ni lazima kuhakikisha kuwa unamakubaliano au mikataba na mmiliki wa kazi hiyo kinyume na hapo huo ni uharamia na uvunjifu wa Sheria ya Hakimiliki.

Kwa upande wa Mtuhumiwa wa Uazilishaji ambaye ni Msimamizi wa Kampuni ya Sanyiwa Production Bw.Frank Manyama alikiri kufanya kosa la kuzalisha kazi mbalimbali za ndani na nje ya nchi bila ya kuwa na kibali cha wamiliki wa kazi hizo.

Operesheni hiyo sehemu ya majukumu ya COSOTA katika kulinda Hakimiliki za Wasanii. na kazi zote za ubunifu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.