Kamishna wa Idara ya Michezo Zanzibar,Ameir Mohamed Makame akizungumza na Viongozi wa Timu mbali mbali ikiwemo Timu ya Mlandege,Miembeni, Ram Sqad pamoja na Vijana wa Uncle katika Ukumbi wa Wizara ya Habari,Vijana Utamaduni na Michezo, Migombani,Wilaya ya Mjini.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Ndugu Fatma Hamad Rajabu amewataka viongozi wa timu mbali mbali kuhamasisha nidhamu kwa washabiki wao pamoja na kusimamia vyema viwanja vya michezo.
Akizungumza kwa Niaba, Kamishna wa idara ya Michezo Zanzibar Ameir Mohamed Makame wakati wa kujadili mechi baina ya Timu ya Miembeni na Mlandege ambazo zinatarajia kupambana tarehe 16/05/2025 wakati wa Uzinduzi wa Uwanja wa Maisara.huko Wizara ya Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo,Migombani. Wilaya ya Mjini.
Alisema ni vyema kuimarisha nidhamu na maadili wakati wa michezo kwa kushangiria kwa furaha sio kutumia lugha chafu za matusi, kuvaa vijora,vinavyowadhalilisha akinamama kufanyafujo, pamoja na nyimbo za kuhamasisha matumizi ya dawa ya kulevya.
"Ondoweni migogoro tuwe na hamasa ya Michezo timu za mitaani zirudi kwenye ligi ili mechi zirudi kama zamani ndio lengo la serikali yetu kuimarisha michezo '' alisema Kamishna Ameir.
Alieleza kuwa michezo ni chanzo cha furaha ,afya njema na kuunganisha watu wa rika na jinsia zote ikitumika vyema huleta utulivu kuimarisha usalama na kukuza vipaji na kupelekea kuwa chanzo cha ajira Kwa Vijana .
aidha alifahamisha kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Husein Mwinyi ameweka miundombinu bora katika viwanja vya michezo ili kuweza kuibua vipaji kwa vijana wake hivyo iko haja ya kuvitunza ili kuwa wazalendo wa kweli kwa taifa lao.
Nae Kamishna Mkuu wa Kinga Tiba na Kurekebisha Tabia Juma Abraham Zidikheiry alisema vijana wengi wanajiingiza katika matumizi ya dawa ya kulevya kutokana na msukumo rika pamoja na migogoro ya familia jambo ambalo huchangia vijana kukosa malezi bora.
Alieleza kwamba dawa za kulevya zinazotumiwa zaidi ni bangi ikifuatiwa shisha, heroun, mirungi, cocaine pamoja na dawa tiba zenye asili ya kulevya ‘Methamphetamine’.
Alifahamisha kwamba Tatizo la Dawa za kulevya Zanzibar inakadiriwa kuwa na watumiaji 9000 ikiwa wengi wao ni Vijana kati ya umri wa miaka 9 hadi 45, Kwa njia ya kujidunga sindano 2,735, maambukizi ya ukimwi miongoni mwa waraibu wanaojidunga ni asilimia 36, maambukizi ya homa ya ini asilimia 60 ,Kifua kikuu asilimia 11 wakati katika jamii yalikuwa ni asilimia 0.2.
Kwa upande wa Mkuu wa Intelijensia wa Madawa ya Kulevya, Haji M. Omar alisema tatizo la dawa za kulevya ni uhalifu unapangwa kwa siri kwa mitandao ya wahalifu wakubwa, wakati na wadogo au vikundi vinavyojipanga.
Alisema Dawa za kulevya ni kemikali ambazo mtu akizitumia huadhiri Mifumo wa fahamu Kwa kuleta vipumbaza ,vileta njozi pamoja na vichangamshi.
Alieleza kuwa hakuna tafiti zinazoonyesha idadi ya watu wanaotumia bangi nchini hivyo Iko haja ya kuchukuwa tahadhari na hatua za makusudi ili kuokoa Taifa lisijeangamia .
Nae Viongozi hao walisema watakuwa mabalozi wazuri kwa kufikisha ujumbe huo wa suala zima la nidhamu kwa wachezaji na washabiki wao kiujumla ili miundombinu ya viwanja ibaki kuwa salama .
Alisema watahakikisha wanatoa muongozo na utaratibu mzima kwa washabiki wao kuachana na nyimbo zisizostahiki kwa Jamii ikiwemo nyimbo ya Njoo Miembeni, Matusi na fujo uvaaji wa vijora pamoja na kutoa tahadhari ya kuingia viwanjani na uraibu wa aina yoyote ili kutunza mazingira yaliyopo.
Kiongozi wa Ram Sqad, Hafidh Othman Jabu , akielezea changamoto wanazozikabili kwa washabiki wao (wa pili kushoto ) Mudathir Yahya Rashid pamoja na Sabra Abdallah Bakari katika ukumbi wa Wizara ya Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo, Migombani, Wilaya ya Mjini.
IMETOLEWA NA KITENGO CHA HABARI. WHVUM.
No comments:
Post a Comment