Habari za Punde

Wajasiriamali Kuwezeshwa Kupata Elimu ya Mafunzo ya Ujasiriamali Ili Kuweza Kujiwezesha.

Na. Mwashungi  Tahir                   Maelezo     30-6-2021.

WAZIRI wa Nchi Afisi ya Rais Kazi Uchumi na Uwekezaji Mhe.Mudrik Ramadhani Soraga amesema Idara ya Uwezeshaji kiuchumi ina lengo la kuwapatia elimu na mafunzo wajasiriamali  ili waweze kujiongeza katika maisha yao.


Ameyasema hayo huko katika ukumbi wa Golden Tulip  Malindi wakati akifunga shindano la mpango wa biashara kwa wajasiriamali na kuwataka elimu waliyokuwa nayo waiendeleze.


Amesema  lengo lakupatiwa elimu na mafunzo  wajasiriamali hao ni kuwashajihisha kuingia katika ujasiri pamoja na kuwasaidia kwa kuwawezesha kupata mitaji ili kujiendeleza katika shughuli zao za maisha.


Aidha  amesema lengo ni kukuza ubunifu   kwa wajasiriamali wadogo na wa kati  katika sekta ya Teknohama  IT , Utalii na usarifu wa mazao pamoja na mafunzo ya uwokaji  ili kuweza kutatua changamoto za ajira na kuongeza kasi ya mafanikio Zanzibar.


Pia amesema  kutokana na ukosefu wa ajira kwa vijana Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeweka kituo cha kulea wajasiriamali  na kuchukua juhudi katika kubuni nyenzo za miradi tofauti ya kuwawezesha vijana ili waweze kuibua fursa zilizopo katika sekta mbali mbali kwa kuondokana na changamoto za ajira.


Nae Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu Uwezeshaji  na kiuchumi Ameir Haji Sheha  amewataka wajasiriamali  kukuza vipaji vyao ili waweze kujiwezesha kiuchumi na kuacha kuwa tegemezi.


Nao wajasiriamali wa mafunzo hayo wameishukuru Serikali kwa jitihada wanazozichukua katika kuwawezesha kwa kujiinua kiuchumi ambapo mshindi wa kwanza katika shindano hilo ni Nassor Abdullah Nassor katika mradi wa kugundua  gesi Rock tech service kati ya washindi kumi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.