Nahodha wa timu ya Netiboli
ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Jane Thawe akimiliki mpira wakati wa
mchezo dhidi ya Timu ya Tume ya Walimu ambao umechezwa leo Oktoba 25, 2021 na
kuingia hatua ya robo fainali katika Mashindano ya Michezo ya Wizara na Idara
za Serikali Tanzania (SHIMIWI) yanayoendelea mjini Morogoro.
Na Mwandishi Wetu, Morogoro
Timu ya Netiboli ya Wizara
ya Utamaduni, Sanaa na Michezo imeingia hatua ya robo fainali katika Mashindano
ya Michezo ya Wizara na Idara za Serikali Tanzania (SHIMIWI) yanayoendelea mjini
Morogoro.
Timu hiyo imefika hatua hiyo
baada kuifunga timu ya Netiboli ya Tume ya Waalimu leo Oktoba 25 kwa jumla ya
magoli 37:08 huku waakicheza mchezo
mzuri wa kuonana vema kwa kufuata maelekezo ya mwalimu wao Alice Choaji ambaye amesema nia yao ni kuchukua ubingwa
wa mashindano hayo.
“Timu ipo vizuri na
wachezaji wanaendelea k kufuata maelekezo vizuri tuliyofundishana wakati wote
wa mazoezi, kwa kweli wanatia moyo maana kila tunapofanya mazoezi kujiaandaa na
michezo wanaendelea kuwa bora zaidi” amesema mwalimu huyo.
Timu zilizoingia hatua ya
robo fainali katika da kundi B ni Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na
Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi na kuzibwaga nje ya mashindano timu za Tume ya
Walimu, Wizara ya Nishati na timu ya Wakala wa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi
(OSHA).
Siri kubwa ya ushindi wao ni
wachezaji wakati wote kuwa makini kuzingatia na kuzifuata kanuni za mashindano
hayo ambapo wachezaji pamoja na viongozi wa timu walifuata barabara ikiwemo
kutumia lugha ya kiungwana wakati wote wa mchezo kwani hairuhusiwi kutoa lugha
chafu ya matusi au kashfa kwa mwamuzi au kiongozi au mchezaji mwenzake wakati
wote wa mashindano hatua iliyowafanya waonane vyema na kutimiza lengo lao kama
timu.
Kuimarika kwa timu hiyo na
kufanya mazoezi ya wachezaji imewafanya miili kuimarika kimchezo zaidi na kuwafanya
wawe katika hali bora zaidi ya kucheza
vema katika hatua ya makundi ambapo mchezo unachezwa kwa muda wa dakika
40 kwa michuano ya awali na kuwafanya waweze kuhimili ushindani wa robo fainali
ambapo mchezo utachezwa dakika 60.
Pia Mwalimu Alice amesema
ushindi wao ununachagizwa na ushirikiano mzuri kati ya viongozi wa Wizara na
wachezaji ambapo amewashukuru Viongozi hao wakiongozwa na Katibu Mkuu Dkt.
Hassan Abbasi ambaye amewakilishwa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu
Bw. Bernard Marcelline ambaye mara zote amekuwa na timu bega kwa bega wakati
wote wa mashindano hayo.
Aidha, Mwalimu Alice
amewataka wachezaji hao wasiridhike na matokeo hayo bali wakaze mwendo na
kujiandaa ipasavyo na michezo inayofuata ili kupata ushindi zaidi ambao kwao
hiyo ni hatua njema na wannadhamiria kuwa na timu ya kudumu ya Wizara itashiriki
mashindano mbalimbali yanayosimamiwa
Chama cha Mpira wa Netiboli nchini (CHANETA) pamoja na mabonanza mbalimbali.
No comments:
Post a Comment