Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj.Dk.Hussein Ali Mwinyi Ameshiriki Sala ya Ijumaa.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi (kulia) akiwasalimia Wananchi na Waumini wa Dini ya Kiisalmu baada ya Sala ya Ijumaa Masjid Fatma Kibanda Hatari Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi,kwa Sheikh Mohamed Ali.
Waumini wa Dini ya Kiislamu na Wananchi wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) alipokuwa  akiwasalimia leo baada ya Sala ya Ijumaa masjid Fatma Kibanda Hatari, kwa Sheikh Mohamed Ali Wilaya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi (katikati) pamoja na Viongozi na Waumini na Wananchi wakiitikia Dua iliyoombwa na Mufti wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar kabi (kushoto) baada ya sala ya Ijumaa masjid Fatma Kibanda Hatari, kwa Sheikh Mohamed Ali Wilaya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi.
Waumini wa Dini ya Kiislamu na Wananchi wakiitikia Dua iliyoombwa na Mufti wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar kabi (hayupo pichani ) baada ya sala ya Ijumaa katika Masjid Fatma Kibanda Hatari, kwa Sheikh Mohamed Ali, Wilaya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi leo. [Picha na Ikulu] 12/Novemba/2021.
 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi amesisitiza haja ya wananchi kudumisha amani na utulivu uliopo nchini, kwa kigezo kuwa ndio msingi wa maendeleo ya nchi.

Alhaj Dk. Mwinyi amesema hayo, wakati alipojumuika pamoja na waumini wa Dini ya Kiislamu katika sala ya Ijumaa iliofanyika Masjid Fatma, Kibanda Hatari kwa Sheikh Mohamed Ali, Jijini Zanzibar.

Amesema  ili Taifa liweze kupata maendeleo, kuna umuhimu mkubwa wa jamii kudumisha amani, umoja na mshikamano uliopo.

Aidha, amewakumbusha Viongozi na watendaji umuhimu wa kuwajibika katika maeneo yao ya kazi, kila mmoja kwa nafasi yake, sambamba na kutilia mkazo  suala zima la uadilifu katika maeneo ya kazi, ikiwemo utoaji wa huduma za jamii kwa wananchi.

Mapema Khatibu wa Sala hiyo ya Ijumaa, Sheikh Omar Abdi aliwataka waumini kushikamana na kuendelea kuitunza amani na utulivu uliopo nchini unaotokana na juhudi za Viongozi za kuwaunganisha wananchi.

Aidha, amesema wananchi wana jukumu kubwa la kuwatii viongozi walioko  madarakani sambamba na kuwajibika ipasavyo katika majukumu yao na kuwa waadilifu ili nchi iendelee kupata neema.

                                                                                                         

Kitengo cha habari,

Ikulu Zanzibar

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.