Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Hussein Ali Mwinyi alimpongeza Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Samia
Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiunga mkono na kuisaidia Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar.
Rais Dk. Mwinyi alisema kuwa katika uongozi wa Rais Samia
Tanzania imepiga hatua kubwa za maendeleo.
Sambamba na hayo alitoa pongezi kwa Watanzania kwa kuendelea
kumuombea dua kwani mambo anayofanya Rais Samia ni makubwa sana.
Aidha, Rais Dk. Mwinyi alitumia fursa hiyo kuipongeza UWT kwa
wazo zuri walilokuja nalo na pia
kushirikiana na Jumuiya zote za CCM kufanikisha jambo hilo kwa msingi kuwa ni
lao wote.
Mapema uongozi wa UWT ulimpongeza Rais Dk. Mwinyi kwa juhudi kubwa anazozichukua katika uongozi wake sambamba na kufanya mageuzi makubwa ya kiuchumi hasa uchumi wa Buluu katika uongozi wake kama Ilani ya CCM ya mwaka 2020-2025 ilivyoelekeza
Kitengo cha habari,
Ikulu Zanzibar.
No comments:
Post a Comment