Na.Raya Hamad -- OMKR
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Mh
Dkt Saada Mkuya Salum ameishauri Kamati ya ya utekelezaji wa mkakati wa kuandaa
mpango kazi wa kitaifa kutoka Taasisi ya Mwalim Nyerere kuhakikisha utafiti
wanaoufanya unaigusa Zanzibar kwenye maeneo muhimu
Dkt Saada ameyasema hayo alipokutana na baadhi ya
wajumbe wa kamati hiyo ofisini kwake Migombani walipofika kujitambulisha na
kuelezea dhamira yao yenye lengo kufanya maandalizi ya utafiti kuelekea kuandaa
mpango huo unaotegemewa kuanza mwezi Januari mwaka 2022
Ameshauri kuwa ni vyema utafiti kuyagusia maeneo ya visiwa
vya Unguja na Pemba kulingana na nafasi yake bila kusahau na kuangalia mila,
tamaduni na mazingira yake kwa kuhakikisha tafiti hizo zinagusa masuala ya
usawa wa kijinsia ukizingatia kuwa Zanzibar ina eneo dogo kulinganisha na Tanzania
Bara
“Ili uweze kuziona changamoto za Zanzibar ni muhimu
kuekewa eneo maalumu katika mpango kazi huo unaoandaliwa pamoja na kuweka
mifano hai itakayoonesha hali halisi ilivyo kulingana na utafiti kwani tatizo
la udhalilishaji ni kubwa hivyo ni vyema kufahamu kiini cha tatizo” alisisitiza
Dkt Saada
Dkt Saada ambae pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa
Wawakilishi Wanawake Zanzibar UWAWAZA ameishukuru kamati hio kwa kumuona kuwa
ni mmoja kati ya mwanaharakati na kiongozi wanaoshiriki maumivu ya wanawake
wanaopinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji ambapo ameahidi Ofisi yake na
mwenyewe binafsi itatoa ushirikiano wa kutosha
Nae Dkt Tatu Nyange Mjumbe wa Kamati hio amesema Serikali
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeingia mkataba na Taasisi ya Mwalim
Nyerere ili kuandaa Mpango kazi wa Kitaifa wa utekelezaji wa maamuzi ya Baraza
la Usalama la Umoja wa Mataifa nambari 1325 yanayohusu ajenda ya Wanawake Amani
na Usalama
Amemueleza Dkt Saada kuwa makubaliano hayo
yanasisitiza kuandaa mpango kazi kama ni muongozo kwa ajili ya wanawake, Amani
na usalama na ifikapo Mwezi wa Januari itakuja kamati maalum ya utafiti na
hivyo uwepo wao ni kuja kuandaa mazingira kufahamu kina nani watawahusisha na
kufikia malengo kwa urahisi
Aidha Afisa utafiti Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Dkt
Salum Ahmeid ambae ni mjumbe wa kamati hio anaeiwakilisha Zanzibar amesema tayari
kamati hiyo imeshaanza kazi katika Mkoa wa Kusini Pemba na kwa Unguja
itahusisha Mkoa wa Mjini Magharibi ambapo Tanzania Bara itahusisha mikoa 10.
No comments:
Post a Comment