Habari za Punde

Shamrashamra za maadhimisho ya miaka 58 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar zaanza na usafi wa mazingira kisiwani Pemba

MKUU wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, akizungumza na wananchi wa mkoa huo, huko Wilaya ya Micheweni mara baada ya kumalizika kwa zoezi la ufanyaji wa usafi wa mazingira, ikiwa ni shamrashamra za maadhimisho ya miaka 58 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MBUNGE wa Jimbo la Tumbe Amour Khamis Mbarouk akifagia katika majani huko Micheweni wakati wa usafi wa mazingira, ikiwa ni shamrashamra za maadhimisho ya miaka 58 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MKUU wa Wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya, akitia taka katika bero maalumu kwa ajili ya kwenda kutupwa wakati wa ufanyaji wa usafi huko Micheweni, ikiwa ni shamrashamra za maadhimisho ya miaka 58 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MKUU wa Wilaya ya Chake Chake Abdalla Rashid Ali, akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Chake Chake walioshiriki katika usafi wa Mazingira katika barabara ya kuelekea uwanja wa ndege wa Pemba, ikiwa ni shamrashamra za maadhimisho ya miaka 58 ya Mapinduzi matukufu ya zanzibar.(PICHA NA HANIFA SALIM, PEMBA)

MKUU wa Wilaya ya Chake Chake Abdalla Rashid Ali, akikata majani katika eneo la Mabaoni Wilaya ya Chake Chake wakati wa usafi wa mazingira ikiwa ni shamrashamra za maadhimisho ya miaka 58 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar.(PICHA NA HANIFA SALIM, PEMBA)

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.