Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa akipokelewa na baadhi watumishi wa Wizara hiyo mara baada ya kuapishwa Januari 10, 2022 Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma kushika wadhifa huo.
Na Eleuteri Mangi,
WUSM-Dodoma
Waziri wa Utamaduni, Sanaa
na Michezo Mhe. Mohamed Mchengerwa ameripoti Ofisini kwake Mji wa Serikali
Mtumba mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Mhe.
Samia Suluhu Hassan Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Mhe. Mchengerwa amepokelewa
na watumishi wa Wizara hiyo wakiongozwa na Naibu Waziri Mhe. Pauline Gekul na
Katibu Mkuu Dkt. Hassan Abbasi tayari kwa kuanza kazi ambayo Mhe. Samia Suluhu Hassan
alimteua Januari 8, 2022 kushika wadhifa huo.
Uteuzi wa Mhe. Mchengerwa
unafuatia mabadiliko ya Baraza la Mawaziri ambayo ameyafanya Rais Mhe. Samia
Suluhu Hassan siku ya Jumamosi na kuapishwa Januari 10, 2022 kushika wadhifa
huo na kuchukua nafasi ya Waziri Innocent Bashungwa ambaye amehamishiwa Ofisi
ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
Aidha, Naibu Katibu Mkuu wa
Wizara hiyo Bw. Said Othman Yakubu pia ameripoti wizarani hapo tayari
kutekeleza majukumu yake ikiwemo kusimamia sekta za Utamaduni, Sanaa na Michezo
ambazo ni nguvu laini (soft power) ya taifa na sekta zinazowapa furaha
Watanzania.
Katika hafla hiyo ya
kuwaapisha viongozi, Mhe. Rais amewaapisha pia Manaibu Waziri, Makatibu Wakuu
pamoja na Manaibu Katibu Wakuu.
No comments:
Post a Comment