Habari za Punde

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Amekutana na Kuzungumza na Balozi wa China Nchini Tanzania.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla  akizungumza na Balozi mpya wa China Nchini Tanzania Bi Chen Mingjian aliefika kwa mazungumzo na kujitambulisha ofisini hapo.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla akizungumza na Balozi  mpya wa Jamhuri ya Watu wa China Nchini Tanzania Mhe.Chen Mingjian (kulia kwake) alipofika Ofisini kwake Vuga kwa mazungumzo na kujitambulisha.

Na Ali Muhammed Shaaban.OMPR. 

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaongeza mashirikiano yaliyopo  na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China  ili kuleta manufaa kwa pande zote mbili.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla  ameeleza hayo Ofisini kwake Vuga alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi mpya wa China Nchini Tanzania Bi Chen Mingjian alipofika Ofisini kwake leo kwa mazungumzo na kujitambulisha ofisini hapo. 

Mhe hemed amesema mashirikiano kati ya Nchi hizo mbili ni ya muda mrefu tokea mwaka 1964 ambapo China imekuwa ikitoa misaada katika nyanja mbali mbali kwa serikali ya mapinduzi ya Zanzibari  kiwemo Afya, na mambo mengine.

Aidha Mhe. Hemed ameeleza kuwa katika mazungumzo hayo wamekubaliana kuweka utaratibu Mzuri wa kubadilishana uzoefu kwa wataalamu wa Sekta mbali mbali  Nchini kwa ndugu zao wa China kutokana na ubobezi waliokuwa nao .

Sambamba na hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amemshukuru Balozi huyo kwa mashirikiano ya karibu na Zanzibar hasa kwa msaada wa Chanjo ya Uviko 19 aina ya Sinovac walioitoa ambapo ameeleza kuwa wazanzibaari na watanzania kwa ujumla wamenufaika na chanjo hio

Katika hatua nyengine Mhe. Hemed  ameialika  jamuhuri ya watu wa china kuendeleza uwekezaji  nchini kupitia miradi mbali mbali kwa maendeleo ya nchi zote mbili

Nae Balozi wa Chini Tanzania Bi CHEN MINGJIAN  amemuhakikisha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kuendeleza mashirikiano yaliyopo baina ya Nchi hizo mbili  kama ilivyoasisiwa tokea mwaka 1964 na kueleza kuwa yeye ana wajibu wa kuendeleza mashirikiano hayo na kuangalia njia mbali mbali za kunufaisha mataifa hayo.

 Aidha Balozi MINGJIAN amemshukuru Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwa mashirikiano anayoendelea kumpatia Balozi Mdogo wa China aliyopo Zanzibar hali hiyo inaonesha namna Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inavyokuza Diplomasia kwa Mataifa mbali mbali.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.