Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akifungua Kikao cha Baraza la Wafanyakazi, Ofisi ya Makamu wa Rais leo Machi 30, 2022 jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga akitoa neno la ukaribisho kwa mgeni rasmi wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi, Ofisi ya Makamu wa Rais leo Machi 30, 2022 jijini Dodoma.
Viongozi na wafanyakazi Ofisi ya Makamu wa Rais wakiimba wimbo wa ‘Solidarity Forever’ kabla ya kufunguliwa kwa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi hiyo uliofanyika jijini Dodoma leo.
Mgeni rasmi Waziri wa
Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo
(waliokaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na wafanyakazi wa
Ofisi hiyo mara baada ya kufungua Kikao cha Baraza la Wafanyakazi leo Machi 30,
2022 jijini Dodoma.
(PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS)
Waziri wa Nchi Ofisi ya
Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) amewapongeza wafanyakazi wa Ofisi ya
Makamu wa Rais kwa utekelezaji wa majukumu yao ikiwemo utatuzi wa hoja 11 za
Muungano ndani ya kipindi cha mwaka mmoja.
Ametoa pongezi hizo
wakati akifungua Kikao cha Baraza la Wafanyakazi, Ofisi ya Makamu wa Rais cha
kupitisha Bajeji ya Utekelezaji wa
Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kilichofanyika leo Machi, 2022
jijini Dodoma
Akizungumza na
wafanyakazi hao Dkt. Jafo aliwataka kuendeleza juhudi hizo ili wananchi wapate
uelewa zaidi kuhusu umuhimu wa Muungano na masuala ya Mazingira.
Pia, Dkt. Jafo alitoa
pongezi kwa wafanyakazi wa Ofisi hiyo kwa kuwajibika ipasavyo katika sekta ya
mazingira ikiwemo kusimamia kampeni mbalimbali zikiwemo ‘Soma na Mti’ ambayo
inahusisha wanafunzi ngazi ya shule za msingi hadi vyuo kupanda miti na hivyo
kuifanya nchi yetu kuwa ya kijani.
“Kikubwa zaidi niwape
moyo watumishi mmefanya kazi nzuri sana, sasa twendeni na spirit (moyo) tuendeleze upendo tulio nao maana bila upendo hakutakuwa
na mafanikio,” alisisitiza Jafo.
Waziri huyo alisema vikao vya Baraza la Wafanyakazi ni muhimu katika kujadili
masuala mbalimbali ya wafanyakazi kwa upana kwa kuzingatia haki, weledi ikiwa
ni pamoja na kujadiliana changamoto za kiutendaji na hatua za kukabiliana nazo.
Aliongeza
kuwa vikao hivyo vinalenga kudumisha utamaduni wa kufanya kazi kwa pamoja,
bidii na maarifa ili kuleta ufanisi katika kutekeleza majukumu ya Ofisi na
Taifa kwa ujumla.
Hivyo aliwataka wafanyakazi kujadili suala la Bajeti kwa kina na
ikiwa zipo changamoto zilizobainishwa mwaka wa fedha uliopita zijadiliwe ili
ziweze kutafutiwa ufumbuzi ili kurahisisha Utekelezaji wa Bajeti ya Mwaka wa
fedha ujao.
“Ninaamini
Bajeti hii imejikita katika kuwezesha, kudumisha Muungano wetu na imezingiatia
masuala ya uhifadhi wa mazingira yetu unaosimiwa na Ofisi hii na pia niwaombe wajumbe
boresheni utendaji kazi ili Ofisi hii iwe mfano wa Taasisi na Wizara zote
katika utekelezaji wa majukumu yetu kwa kuzingatia umuhimu wa Ofisi hii,” alisisitiza
Jafo.
No comments:
Post a Comment