Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro amewaagiza Makamanda wa
Polisi nchi nzima kufanya operesheni ya mwezi mmoja ya kudhibiti makosa ya
usalama barabarani ambayo kwa kipindi cha mwezi wa tatu mwaka huu yameonekeana
kuongezeka.
IGP amesema hayo jijini Dar es salaam wakati akizungumza kwenye kikao
kazi na Makamanda wa Polisi wa mikoa ya Dar es salaam, Morogoro, Pwani, Rufiji
ma RTOs na DTOs pamoja na Wakuu wa Operesheni kutoka kwenye mikoa hiyo.
Aidha, katika kikao kazi hicho IGP Sirro ametoa agizo kwa wananchi
kuendelea kufuata sheria za usalama barabarani kwa lengo la kuepusha ajali
zinazoweza kuepukia.
Katika hatua nyingine IGP Simon Sirro amekutana na kuzungumza na balozi wa
Palestina nchini Tanzania Mhe. Hamdi Mansour Abuali aliyemtembelea ofisini
kwake Makao Makuu Ndogo ya Jeshi hilo na kujadiliana mambo mbalimbali kuhusiana
na masuala ya usalama na ushirikiano.
No comments:
Post a Comment