Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Othman Masoud Othman, leo Mei 25,2022 amekutana na kufanya mazungumzo na Viongozi wa Chama cha Walimu Zanzibar (ZATU) pamoja na Viongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar (WEMA).
Kikao hicho ambacho ni muendelezo wa ziara ya Makamu wa Kwanza wa Rais iliyoanza mapema mwezi Machi mwaka huu katika sekta ya Elimu Zanzibar, yenye lengo la kutambua changamoto na kuzitafutia ufumbuzi wake kimefanyika katika Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar iliyopo Migombani Mkoa wa Mjini Magharib Unguja.
No comments:
Post a Comment