Habari za Punde

MAFUNZO YA SENSA KWA WANAMASKANI YA KACHORORA

Mwenyekiti wa Maskani ya Kachorora CCM Kariyakoo Mjini Zanzibar Moh’d Mussa Bakari akimkaribisha mkufunzi wa mafunzi ya Sensa na makaazi ya watu Abdulmajid Jecha Ramadhani  mara baada ya kuwasili ukumbi wa maskani hiyo, (kulia) Mzee wa maskani ya Kachorora  Said Shaabani na (kushoto) Katibu wa maskani hiyo Mtumwa Othman Mselem.
Mratibu wa  sensa ya watu na Makaazi Tanzania Zanzibar Abdulmajid Jecha Ramadhani akitoa mafunzo kwa wanachama wa Kachorora waliofika katika mafunzo hayo.
Wanachama wa maskani ya Kachorora wakifuwatilia mafunzo yanayotolewa na Mratibu Abdulmajid Jecha katika ukumbi wa Maskani ya Kachorora Kariayakoo Mjini Zanzibar.

Mwanachama wa CCM Omar Ramadhan Issa akimuuliza swali  Mratibu wa Sensa na Makakazi ya watu kuhusu mwananchi mwenye zaidi ya nyumba tatu vipi mtuhuyo ataisabiwa katika sensa hiyo.

Picha na Miza Othman-Maelezo Zanzibar.   

Na Khadija Khamis- Maelezo 16/06/2022.

Jamii imetakiwa kushiriki zoezi la sensa ya watu na makaazi ambalo linatarajiwa kufanyika tarehe 23 Agosti mwaka huu.

Hayo ameyasema  Mratibu wa Sensa ya Watu na Makaazi  Tanzania Zanzibar Abdulmajid Jecha Ramadhani wakati akitoa mafunzo kwa wanamaskani ya Kachorora kuhusiana na zoezi la sensa ya watu na makaazi katika mukumbi wa maskan hiyo. 

Amesema zoezi la sensa ni la kitaifa Kila mtu anawajibu wa kuhesabiwa ambae amelala ndani ya  mipaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania .

 

Aidha alifahamisha  kuwa watu wote watakaohesabiwa ambao watalala  usiku wa  kuamkia siku ya sensa katika Kaya zao na iwapo mkuu wa  Kaya atakuwa na kaya zaidi ya moja atahesabiwa sehemu ambayo aliyolala kwa siku ile.


Amesema umuhimu wa sensa ni  kujua idadi ya watu na mahitaji yao na kutathmini upungufu wa huduma za kijamii ikiwemo elimu,Afya ,umeme, maji safi na salama hali ya ajira  miundombinu na kadhalika kwa lengo la kuleta  maendeleo ya  wananchi  .


Alifahamisha kuwa kila mtu anahitaji kushiriki katika sensa ya watu na makaazi kwani kutokushiriki kutasababisha kuwa njima fursa za kupata huduma  watu  wengine .

Nae Katibu wa maskani ya kachorora Mtumwa Othman amesema lengo la kuwapatia mafunzo ya sensa kwa wanachama  wa chama cha mapinduzi ni kuiunga mkono serikali katika zoezi hilo la kitaifa .


Alieleza mafunzo hayo yatasaidia kuwapatia  elimu wanachama hao ili kuwa mabalozi kwa wengine lengo ni kufanikisha malengo ya zoezi hilo.


Nao wanachama  wa maskani ya kachorora wamesema wameridhika na mafunzo ya sense ya watu na makaazi waliyoyapatiwa na watashiriki kikamilifu katika zoezi hilo na kuwataka watu wote washiriki bila ya kujali dini kabila na jinsia na chama kwani  kila mtu anahitaji kuhesabiwa.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.