Habari za Punde

Kikao cha Sita CHA SENSA Kuelimisha Jamii Kujua Mfano wa Masuala ya Msingi.

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa ambae pia ni Mwenyekiti wa Kamati Kuu ya Kitaifa ya Sensa ya Watu na Makazi akifungua Kikao cha Sita  Kamati hiyo kilichofanyika Ukumbi wa Melia Hotel Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Mwenyekiti  Mwenza wa Kamati Kuu ya Kitaifa ya Sensa ya Watu na Makazi ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleman Abdulla akifunga Kikao cha Sita  cha Kamati hiyo kilichofanyika Ukumbi wa Melia Hotel Pwani Mchangani Mkoa wa Kaskazini Unguja
Wajumbe wa Kamati Kuu ya Kitaifa ya Sensa ya Watu na Makazi wakifatilia kwa makini Kikao cha Sita cha Kamati hiyo kilichofanyika Ukumbi wa Melia  Hotel Pwani Mchangani Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amezitaka Wizara za Habari za SMT na SMZ  kuvitumia Vyombo vya Habari katika kuelimisha Jamii kujua Mfano wa Masuala ya Msingi watakayoulizwa katika Zoezi la  Sensa ya  Watu na Makazi ifikapo Agosti 23 Mwaka huu.

Mhe.  Majaliwa ambae pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Kitaifa Sensa ya watu na Makazi 2022 ameyasema hayo katika Kikao cha Sita cha  Kamati hiyo kilichofanyika Ukumbi wa Melia Hotel  Pwani Mchangani Mkoa wa Kaskazini Unguja.

 

Amesema ili kuwaweka tayari Wananchi kukabiliana na Zoezi hilo ni vyema kuwa na ufahamu mapema namna atakavyohojiwa ili kurahisisha na kuondoa hofu kwa Wananchi. 

 

Mhe.  Majaliwa amesema Jamii ya Watanzania inafatilia zaidi Mitandao ya Kijamii hivyo ni vyema kutumia Fursa hiyo kwa kuelekeza nguvu ili kurahisisha Zoezi hilo.

 

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  ameeleza kuwa juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Sekretarieti ni zenye kuthaminiwa ambapo ameipongeza kwa mashirikiano mazuri waliyokuwa nayo kwa pande zote Mbili za Muungano.

 

Aidha Mhe. Majaliwa amemshukuru Muwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalosimamia Idadi ya Watu Duniani (UNFPA) Nchini Tanzania  kwa kuendelea kuunga Mkono kwenye uratibu wa Zoezi hilo na kumuhakikishia kuwa Serikali itaendelea kuwa nao hadi kukamilika kwa zoezi hilo.

 

Kwa upande wake Mwenyekiti Mwenza wa Kamati hiyo Mhe. Hemed  Suleiman Abdulla  amewashukuru Viongozi wa Kitaifa kwa kuonesha Mfano wa Kushajihisha umuhimu wa Sensa ya Watu na Makazi hasa kupitia Ziara ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa kuwafikia Wananchi wa Mikoa yote ya Zanzibar.

 

Aidha amewataka Viongozi wote wa Serikali kuendelea kuhamasisha na kueleza umuhimu wa Zoezi hilo na kupongeza Kampeni ya Viongozi mbali mbali kueneza Vipeperushi kupitia Mitandao ya Kijamii inayoonesha utayari wao wa kushiriki katika zoezi hilo.

 

Samba na hayo Mhe. Hemed ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa  Zanzibar  amezishukuru Taasisi za Kidini na makundi mbali mbali kwa kuendelea kutumia Fursa walizonazo katika kuwahamasisha walio kwenye dhamana zao.

 

Kwa Upande wao Watakwimu Wakuu wa SMT na   SMZ wameeleza kuwa Zoezi la  kupata Makarani na wasimamizi wa Sensa limekwisha kamilika ambapo hatua inayoendelea sasa ni kukamilisha Mafunzo kwa Makarani kutoka katika Shehia na Kata.

 

Wameeleza kuwa        Mafunzo wanayopatiwa Watendaji hao ni kuhakikishaZoezi la Sensa ya Watu na Makazi linafanikiwa na kuwataka washiriki kuwa makini kipindi cha  Mafunzo ili kufaulu vyema Mitihani na hatimae kufanikisha vyema Zoezi hilo.

 

Abdulrahim Khamis

Afisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

30/07/2022

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.