Habari za Punde

Shirika la Afya Duniani (WHO) latoa msaada wa vifaa vya afya kwa Hospitali za Zanzibar

Mwakilishi Mkaazi kutoka (WHO)  Tanzania Dr. Zabulon Yoti akizungumza na mkurugenzi wa Wizara ya Afya  hayupo pichani wakati walipofika katika Afisi ya Wizara hiyo Mnazimmoja Mjini Zanzibar. Picha na Miza Othman- Maelezo Zanzibar.
Naibu Waziri wa Afya Zanzibar, Mhe Hassan Khamis Hafidh na Mwakilishi Mkaazi wa WHO Tanzania  pamoja na uongozi wa wizara hiyo wakikabidhiana Vifaa 56 kwa ajili ya matumizi ya wagonjwa  wa Hospitali za Unguja na Pemba yaliyofanyika Wizara ya Afya Mnazimmoja Mjini Zanzibar. Picha N Miza Othman-Maelezo Zanzibar.

Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Hassan Khamis Hafidh  akiwa katika picha ya pamoja  ya pamoja na uongozi kutoka WHO  na wizara ya Afya Zanzibar.

Picha N Miza Othman-Maelezo Zanzibar.

 Na Bahati Habibu    Maelezo   2/9/2022

 

Naibu Waziri wa Afya Hassan Khamis Hafidh amesema Shirika la Afya Duniani (WHO) limekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha sekta ya afya inaimarika nchini na kutoa huduma kwa wananchi. 

 

Akizungumza wakati wa kupokea msaada wa mashine za kupumulia huko ofisini kwake Mnazimmoja amesema msaada huo wenye thamani ya zaidi milioni 77 ambao utasaidia wagonjwa wanaosumbuliwa na maradhi ya kushinda kupumua wanaofika kupata huduma katika  vituo na Hospitali mbali mbali. 

 

Amesema tatizo la kupumua limekuwa likiwasumbuwa wananchi wengi hasa wagonjwa pumu na shindikizo la damu hivyo mashine zitasaidia kuuokoa maisha ya jamii inayosumbuka tatizo hilo .

 

Aidha  ameliomba Shirika hilo kuisaidia Zanzibar kupunguza vifo vya mama na mtoto na maradhi ya presha, sukari na saratani ambayo yamekuwa kuongezeka kila siku. 

 

Nae Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Afya Duniani nchini Tanzania Dr Zabulon Yoti amesema shirika lipo tayari kushikrikiana na Serikali  ili kuhakikisha kwamba inapunguza na  kuondosha vifo vinavyosababishwa na maradhi yasiyoambukiza ambaoyo yamekithiri nchini.


Aidha amesema Shirika hilo litaendelea kutoa msaada wa dawa na vifaa tiba kwa Serikali  kwa lengo la kuimarisha sekta ya afya nchini.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.