Habari za Punde

Wazazi watakiwa kuwasomesha watoto wao masomo ya dini

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Al-hajj Hemed Suleiman Abdulla akiwasalimia watoto waliojumuika katika Ibada ya Swala ya Ijumaa Masjid NABAWII Mombasa Mbuyu Mnene..  Leo tarehe 23/09/2022
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Al-hajj Hemed Suleiman Abdulla akiwa katika picha ya pamoja na watoto waliojumuika katika Ibada ya Swala ya Ijumaa Masjid NABAWII Mombasa Mbuyu Mnene..  Leo tarehe 23/09/2022
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Al-hajj Hemed Suleiman Abdulla akiwasalimia waumini wa Masjid NABAWII Mombasa Mbuyu Mnene baada ya Ibada ya Swala ya Ijumaa  Leo tarehe 23/09/2022.


Na Ally Mohammed 

Wazazi wametakiwa kuwasomesha vijana ili kupata viongozi bora na wenye kuweza kutoa fatwa kwa kutumia sheria za dini

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla ametoa wito huo alipojumuika na Waumini katika Masjid NABAWII Mombasa Mbuyu Mnene wilaya ya magharibi “B” unguja

 Ameeleza kuwa ni wajibu wa kila mzazi na mlezi kuhakikisha anawapatia elimu vijana wake   ili kuweza kuwa vijana bora wenye kutambua mema na maovu katika nchi

Mhe. Hemed amesema kila mzazi ana jukumu la  kuwaanda vijana kuwa viongozi bora wa baadae ambao watasimamia maslahi ya wazanzibari pamoja na kuwa wanazuoni bora.

Alhajj Hemed amewataka waumini na wananchi kwa ujumla kuwasimamia viajna ili kuweza kuondosha chanagamoto zinazoikabili nchi kwa sasa ikiwemo tatizo la madawa ya kulevya na udhalilishaji.

 

Amesema kuwa ni lazima kila mzazi na mlezi kufanya kila linalowezekana kuwaandaa vijana kwenye kupata elimu bora ambayo itawasaidia hapa duniani na kesho Ahera pamoja na kupata viongozi kwa maslahi ya nchi yetu.

Kwa upande wake Imamu wa Msikiti huo  Sheh. SAADAT IMAMU  amewataka Waumini na wazanzibari  kurudi kwa Allah na kuacha yale yote amabyo yanaweza kuiletea balaa nchi yetu.

Amesema ni wajibu kwa kila muumini kufanya  ibada huku akitarajia ujira mkubwa kutoka kwa Allah na kuwataka kufika kwa wakati katika swala zote ikiwemo swala ya ijumaa ili kupata fadhila za allah (S.W)

Wakati huo huo Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Alhajj Hemed amepata fursa ya kumjulia hali Mfanya biashara maarufu nchini MOHAMMED RAZZA nyumbani kwake kibweni wilaya ya magharibi “A” unguja

Amemtaka mfanya biashara huyo kuwa na subra kwa kipindi hichi cha kuumwa kwake na kumuombea duwa kwa mwenyezi mungu kuweza kupona kwa haraka ili aweze kuendelea na majukumu yake ya kawaida ya ujenzi wa taifa.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.