Habari za Punde

Waziri Mhe Chana Aipongeza TFS Mbio za Magari za Sao Hill

Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Saad Mtambule akimkabidhi kombe bingwa wa Mashindano  Sao Hill Misitu auto Cross Tanzania  The Royal Tour

Na Fredy Mgunda,Iringa.

Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dk Pindi Chana amevutiwa na ubunifu na mawazo  mazuri yaliofanywa na Shamba la Serikali Sao hili kwa kuandaa Mashindano ya mbio za Magari katika msitu huo kwani ni fursa kubwa ya kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo kwenye Shamba hilo.


Balozi Dk Chana ameyasema Hayo wakati akizungumza kwa njia ya simu katika Mashindano  Sao Hill Misitu auto Cross Tanzania the Royal Tour kwa kushirikiana Iringa Motorsports club Tanzania kwa ubunifu huo kwani unaumuhimu mkubwa katika masuala mazima ya kutangaza utalii.


" Haya nimaelekezo ya Rais wetu Samia Suluhu Hassan ambaye alituelekeza kuendelea kubuni vyanzo mbalimbali vya utalii kwani ndio chanzo kimoja wapi katika masuala mazima ya utalii wa aina hiyo wa mashindano ya mbio za mahari au Rally katika misitu yetu ambavyo tunaihifadhi mwenye maeneo yetu ." Alisema dk  Balozi Chana


Aidha alieleza Mkakati wa wizara ni kunatukio masuala ya michezo mbalimbali  ambayo utafanyika  katika maeneo ya hifadhi za Serikali ikiwemo msitu katika eneo la Sao hill.


" Ni jambo zuri na tuendelee kuratibu ili liweze kufanyika mara kwa mara  kadiri Kamati ya maandalizi tutakavyo amua I'll kupata washiriki wengi zaidi." Alisema Waziri huyo


Kwa upande wake Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Sao hill Lucas Sabida alisema wameandaa mashindano mafupi ya mbio za mahari lakini wanampango wa kuandaa mashindano makubwa zaidi.


Alisema lengo la mashindano Hayo ni kuendelea kujitangaza kama Shamba la TFS kwa ajili  kutangaza utalii wa ikolojia na nyuki kupitia utalii wa michezo wa mbio za Magari kutokana na mwitikio kuwa mkubwa kwao Wananchi.


Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Saad Mtambule alisema kuwa wilaya hiyo inamisitu Msingi ambapo wanaziadi ya hekta 100,000 ambayo inatumiwa kwa ajili ya uzalishaji wa mbao pamoja na bidhaa zingine kama Marine boad, Mirunda  na nguzo za umeme.


Alisema mazao Hayo wamekuwa wakiyatumia na kuwasaidia kwa uchumi na mapato kwa mustakabali wa jamii  lakini kupitia Program ambayo ilianzishwa na Rais wa Jamhuria ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan  The Royal Tour.

Moja ya magari ambayo yalishiriki katika Mashindano  Sao Hill Misitu auto Cross Tanzania  The Royal Tour
Moja ya magari ambayo yalishiriki katika Mashindano  Sao Hill Misitu auto Cross Tanzania The Royal Tour
Hizi na zawadi ambao washindi wa Moja ya magari ambayo yalishiriki katika Mashindano  Sao Hill Misitu auto Cross Tanzania  The Royal Tour walipewa

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.