Habari za Punde

Ufunguzi wa Kongamano la Pili la Kumuenzi Marehemu Maalim Seif Shariff Hamad

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa pili wa kumuenzi Marehemu Maalim Seif  uliofanyika hoteli ya Golden Tulip leo tarehe 22.10.2022 . Mkutano huo umeandaliwa na Maalim Seif Foundation na kuwashirikisha wataalamu , wanasiasa , wanadipmomasia na viongozi mbali mbali. 

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa pili wa kumuenzi Marehemu Maalim Seif  uliofanyika hoteli ya Golden Tulip leo tarehe 22.10.2022 . Mkutano huo umeandaliwa na Maalim Seif Foundation na kuwashirikisha wataalamu , wanasiasa , wanadipmomasia na viongozi mbali mbali. 

Baadhi ya washiriki wa Mkutano wa pili wa kumuenzi Marehemu Maalimu Seif Sharif Hamad wakimsikiliza Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, alipozungumza katika ufunguzi wa mkutano wa pili wa kumuenzi Marehemu Maalim Seif  uliofanyika hoteli ya Golden Tulip leo tarehe 22.10.2022 . Mkutano huo umeandaliwa na Maalim Seif Foundation na kuwashirikisha wataalamu , wanasiasa , wanadipmomasia na viongozi mbali mbali. Picha Na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Kitengo cha habari.

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema kwamba wakati nchi inaelekea katika mjadala wa Mageuzi makubwa ya sekta ya elimu ni wajibu kwa Wazanzibari kuwa na tafakuri ya kina juu ya umuhimu wa suala hilo na namna kulifanikisha kwake.

Mhe. Othman ameyasema hayo huko hoteli ya Golden Tulip Kiembesamaki mjini Zanzibar, alipofungua mkutano wa pili wa kumuenzi Maalimu Seif Sharif Hamad ulioandaliwa na Maalim Seif Faoundation  na kuwashirkisha wanataalama, wanasiasa, na wanadiplomasia kutoka ndani na nje ya Tanzania.

Mhe. Makamu amesema kwamba hatua hiyo ni muhimu katika jitihada za pamoja za kujenga khatima njema ya Zanzibar  kielemu kwa kuzalisha vijana wenye maarifa na uwerevu wa kitaaluma hasa kwa vile taifa imara linategemea sana kizazi makini kilichotayarishwa kukabiliana na changamoto zilizopo na zijazo.

Amefahahamisha kwamba hali hiyo ni lazima kwenda sambamba  na kuwepo maridhiano ya kweli, amani na utulivu nchini na kuwepo jitihada kubwa  za kutajenga uchumi imara na kuleta  maendeleo ya kweli  nchini.

Aidha Mhe. Othman amesema kwamba hili hiyo nilazima pia kuziweka katika tafakuri na tathimini sahihi rasilimali za aina mbali mbali zilizopo nchini katika kuijenga Zanzibar kuwa imara  zaidi kupitia elimu itakayotolewa.

Amesema kwamba  kuwepo Zanzibar yenye uchumi imara ni muhimu katika kukabiliana na changamoto mbali mbali zinazokwamisha maendeleo ya nchi.

Mhe. Othman amesema kwamba   katika kukabiliana na hali bora ya kuwatayarisha vijana kielimu ni lazima kwa serikali kutengeneza na kuwepo sera  na uendeshaji bora wa sekta hiyo ya belimu unaosaidiwa na  usimamizi bora sambamba na kuwepo muono sahihi  katika uongozi wa ngazi mbali mbali.

Aidha Mhe Othman amesema kumtayarisha mtoto  kuwa mwerevu kielimu  kutasaidiwa sana na kuwepo makuzi na malezi bora kwa kuzingatia mazingira anayoishi  ikiwemo usomeshaji  na kuwepo na kutumika mitaala bora  huku mwalimu akipewa umuhimu wa kipekee kutokana na uwezo wake wa kumsaidia mwanafunzi kujifunza.

Mhe. Othman amesema kwamba nchi ni lazima ijitahidi  kukubuni mbinu tofauti zitakazosaidia kuhakikisha kwamba  sekta ya elimu inazalisha vijana werevu  watakaokwenda samabamba na mahitaji ya sasa nay a baadaye yanaongozwa na mabadiliko ya sayansi na teknolojia kwa manufaa ya taifa  na kwamba jambo hilo linawezekana kufikiwa ingawa njia za kufikia zinaweza kutafautiana.

 Naye Mhadhiri Mstaafu  wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Issa Shivji, akiwasilisha mada kuhusu uhuru wa elimu kama msingi wa Demokrasia , amasema kwamba huwezi kuwa na elimu bora bila kwepo walimu bora wanaoweza kutengeneza vipaji kwa vijana.

Amesema kwamba walimu ndio wenye uwezo na upeo sahihi wa kukuza vipaji vya wanataaluma na kuzalisha wasomi bora wanaojimani katika kuchangia vyema maendeleo ya taifa lao.

Professa Shevji amesema kwamba wanafunzi wa namna hiyo ndio wenye uwezo wa kujadili  na kudadisi mawazo mbali mbali yaliyopo  na kutoa  mbadala yatakayosaidia vijana kuweza kuchangia upeo wa maendeleo ya nchi yao.

Nao baadhi ya washiriki katika Mkutano huo wamesema kwamba katika kuhakikisha maendeleo bora ya elimu nimuhimu kujadili , kupanga na kuamua kuanzisha mifuko mbali mbali itakayosaida kuwa miundombinu ya kukuza  maendeleo ya sekta ya elimu ili kupata vijana wenye uwezo mkubwa kitaaluma.

Mkutano huo wa Siku mbili ambao ni wa pili umetayarishwa na Maalimu Seif Foundation, na umewakutanisha wananasiasa, wataalamu , wanadiplomasia na wananchi mbali mbali utatajidili mada kadhaa ikiwa ni hatua ya kuenzi Fikra za Marehemu maalum seif Sharif kutokana na mchango wake mkubwa katika kuwaleta wananchi wa Zanzibar na Tanzania kwa jumla  pamoja, kuhubiri amani na mshikamano  pamoja na kuchangia ukuaji wa demokrasia na haki za binaadamu nchini.

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia kitengo cha Habari leo tarehe 22.10.2022.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.