Mmoja ya washiriki waliyofika katika mafunzo ya Kiswahili kwa wageni akichangia mada marabaada ya kupatiwa mafunzo hayo huko ukumbi wa Baraza la Sanaa Mwanakwerekwe mjini Zanzibar.
Picha na Miza Othman- Maelezo Zanzibar.
Na Khadija Khamis Maelezo .29/11/2022. Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana. Utamaduni na Michezo, Fatma Hamad Rashid amesema kuhamasisha utumiaji wa lugha ya kiswahili kwa wageni na wenyeji kutasaidia kufanikisha mpango mkakati wa kitaifa wa kukuza na kuendeleza kiswahili nchini
Hayo ameyasema katika ukumbi wa Baraza la Kiswahili Zanzibar ( BAKIZA ) Mwanakwerekwe,Wilaya ya Magharibi ‘B’ wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tano ya ufundishaji wa kiswahili kwa wageni.
Amesema Serikali tayari imeshafungua milango kwa wageni hivyo Iko haja ya kujua njia Bora ya ufundishaji wa lugha ya kiswahili kwa wageni jambo ambalo litatoa fursa ya kuuendeleza Utamaduni huo kwa ndani na nje ya nchi.
Aidha amesema Zanzibar kuna wataalamu wazuri wa ufundishaji wa lugha ya kiswahili kwa wageni jambo ambalo litasaidia kukirithisha kiswahili kutoka kizazi na kizazi pamoja na kukisomesha kwa wageni .
Alifahamisha kuwa kuna kila ya sababu ya kujivunia kutokana na umahiri mbinu na ustadi wa wakufunzi hao kwa njia bora wanazozitumia kwa wanafunzi wao.
Nae Mwenyekiti wa Baraza la Kiswahili Zanzibar Dkt Saade Said Mbarouk amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo walimu kuwa na njia bora ya ufundishaji wa lugha ya kiswahili kwa wageni na wazawa.
Mafunzo hayo ni ya mara ya kwanza kufanyika hapa Zanzibar na yanatarajiwa kuwa endelevu ili kuhamasisha na kuendeleza utamaduni wa lugha ya kiswahili kwa wageni.
No comments:
Post a Comment