Habari za Punde

Tamashgala Vijana NDOTO AJIRA HUKO SUZA TINGUU

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amewataka Vijana nchini kuzitumia vyema fursa za kutengeneza ajira zinazoanzishwa na serikali ili waweze kufikia ndoto zao za kuwa na ajira za uhakika kwa maendeleo ya na taifa kwa jumla.

Mhe. Othman ameyasema hayo katika Ukumbi wa Dk Ali Mohammed Shen huko Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar ( SUZA) alipozungumza katika Tamasha la Kongamano la vijana la Ndoto ajira lilowakutanisha vijana kutoka ndani nan je ya Tanzania.

Mhe. Makamu amefahamisha kwamba ukosefu wa ajira kwa vijana  ni moja ya changamaoto kubwa  za kijamii inayozikabili nchi nyingi duniani  na zaidi barani Afrika na kwa kiasi kikbwa inachangiwa na mitazamo ya vijana kutegemea kuajiriwa serikali pekee.

Amesema Tamasha hilo la Ndoto- Ajira ni fursa kubwa kwa vijana wa Afrika Mashariki kujionea namna wanavyowasilisha mawazo yao na ubunifu walionao katika Nyanja za biashara na sekta ya  uchumi  wa bluu ili kutimiza malengo yao ya kujiajiri na kuondokana na mawazo ya kuajiriwa serikali kama fursa pekee ya ajira.

Amefahamisha kwamba serikali  kupitia Ofisi ya Rais, Kazi , Uchumi na uwezeshaji wananchi kiuchumi imeunda chombo cha Wakala wa Uwezeshaji wananchi kiuchumi ili kuwasaidia vijana kutimiza ndoto zao kwa kuweza kupatiwa mafunzo  ya ujasiriamali , mikopo na kutafutiwa masoko kwa bidhaa wanazozalisha na kusaidia kukuza pato kwa vijana.

Hivyo Mhe. Othman amesema kwamba serikali kupitria Taasisi zake na kwa kushirikiana na washirika wa maendeleo imeandaa program maalum za kuwawezesha vijana kwa kuwakuza kiujizi kupitia skuli na vyuo vyua Ufundi , vituo vya uwezeshaji ili waweze kuingia katika soko la ajira na kujikwamua kiuchumi na kupunguza tatizo la ajira.

 

Amefahamisha kwamba kufanya hivyo ni jitihada maalumu  za kutafuta suluhisho muhimu  kwa tatizo la ajira kwa kuwaandaa vyema vijana  wenye elimu sahihi , ujuzi na maarifa ya kazi kwa kuweza kujiajiri na kutimiza ndo yao ya ajira.

Mhe. Makamu amesema kwamba hali hiyo ni kutokana na ukweli kwamba serikali inafahamu vyema kundi kubwa la vijana linapaswa kuangaliwa vyema kwa matazamo wa aina yake kwa lengo la kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za kukuza uchumi na kueleta maendeleo nchini.

Amefahamisha kwamba serikali inafanya hivyo kwa kutambua mchango mkubwa wa viajana kwa maendeleo ya taifa hivyo itaendelea kuimarisha uwezo wao katika Nyanja za kujumuisha elimu, sayansi na Teknolojia, ubunifu, uchumi, Sanaa, utamaduni na michezo  ili kuenua ustawi wa maendeleo ya vijana kwa sasa na baadae.

Aidha aliwataka vijana kutambua kwamba muda ni thamani kubwa katika masisha ya mwanadamu na kwamba wanapaswa kuutumia vyema  kwa kujitahidi kujiaanda katika kutafuta mafanikio yao ya kiuchumi na kimaendeleo bila kukata tamaa.

Naye Waziri wa Nchi Afisi ya Rais , Kazi , Uchumi na Uwekezaji Mhe. Mudrik Ramadhan Suraga, amesema kwamba ukosefu wa ajira kwa vijana ni kilio cha muda mrefu na kwamba Ndoto- Ajira wamekuja na mtazamo mpya kuhusu changamoto hiyo kwa vijana.

Amesema kwamba vijana wanaweza kuzitumia fursa mbali mbali zinazoanzishwa katika jitihada za kuwa wabunifu , kutumia elimu na maarifa wanayopatiwa  na hatimae waweze kupata mafanikio katika jitihada zao za kuleta maendeleo.


Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo cha Habari leotarehe 19.11.2022.  

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.