Habari za Punde

Naibu Waziri Mhe. Masanja Agawa Vifaa Tiba Vyenye Thamani ya Shilingi Milioni 14 na Mitungi ya Gesi 100 Magu

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mwanza, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja akimkabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 14 Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya ya Magu, Wilbard Bandolla(kushoto) kwa ajili ya kusaidia watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Magu leo hospitalini hapo.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mwanza, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja akimkabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 14 Mganga Mkuu wa Wilaya ya Magu, Dkt. Maria Kapinga (kulia) kwa ajili ya kusaidia watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Magu leo hospitalini hapo.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Magu, Dkt. Maria Kapinga (kulia) akitoa shukrani kwa Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mwanza, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (wa tatu kushoto) baada ya kukabidhiwa vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 14 kwa ajili ya kusaidia watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Magu leo.

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mwanza, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja akimkabidhi mama mjamzito mojawapo ya mtungi wa gesi kati ya mitungi 100 aliyogawa kwa wanawake wajawazito kwa ajili ya kupunguza shughuli nzito za kutafuta nishati mbadala katika hafla fupi iliyofanyika Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza leo.

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mwanza, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja akiwa ameambatana na Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Magu amegawa vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 14 kwa Hospitali ya Wilaya ya Magu pamoja na mitungi ya gesi 100 kwa wanawake wajawazito.

Akizungumza leo katika hafla ya ugawaji wa vifaa hivyo vyenye thamani ya shilingi 14,575,000 na mitungi ya gesi 100 kwenye Hospitali ya Magu, Mhe. Masanja amesema vifaa hivyo vimetokana na mchango wake binafsi pamoja na mchango wa Doris Mollel Foundation.

Amefafanua kuwa vifaa tiba hivyo vitasaidia kuokoa maisha ya watoto waliozaliwa njiti na pia mitungi ya gesi itasaidia wanawake wajawazito kupunguza shughuli nzito za kutafuta nishati mbadala.

Mhe. Masanja amewaasa wanawake wajawazito kuhudhuria kliniki mara kwa mara ili kujua maendeleo ya mtoto anapokuwa tumboni.

Aidha, Mhe. Masanja amewataka wanawake wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada anazozifanya za kuwaletea maendeleo wananchi wa Tanzania.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya ya Magu Dkt.Maria Kapinga amesema vifaa hivyo vilivyotolewa na Naibu Waziri Masanja vitasaidia kunusuru maisha ya watoto wanaozaliwa kabla ya muda ( njiti).

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.