Habari za Punde

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe.Othman Masoud Amewka Jiwe la Msingi la Ufunguzi wa Tangi la Maji Safi na Salama Masingini,Shamrashamra za Miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar

Na.Mwandishi wa OMKR.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Maoud Othman, amesema kwamba juhudi kubwa zinazofanywa na serikali katika uwekezaji wa kuweka miundombinu kwenye miradi ya maendeleo lazima viongozi na wananchi kuweka mikati imara ya kuitunza ili miradi inayoanzishwa iweze kuwa endelevu.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman ameeleza hayo alipohotubia katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la tangi la maji safi na salama huko Masinginbi Wilaya ya Magharib ‘A’ Unguja ikiwa ni shamra shamra za kutimia miaka 59 tokea kufanyika Mapinduzi ya Zanzibar ya Januari 1964.

Amefahamisha kwamba, hatua ya kuwepo miradi ya aina hiyo ni jitihada za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kulipa umuhimu mkubwa suala la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa kufanya juhudi mbali mbali ikiwemo uanzishwaji wa miradi mikubwa ya maji ili kuondoa kero kwa wananchi lakini kudumu kwa miradi hiyo kunahitajika kuwepo sera bora na mipango madhubuti ya kuitunza miradi inayoanzishwa.

Mhe. Othman amesema kwamba ingawa  baadhi ya  maeneo bado kuna changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji lakini ukamilishaji wa mradi huo   uliohusisha sheheia za Masingini ,  Dole na Dimani, Kwarara Kidutani , Mkorogo, Mfenesini na Maungani itasaidia sana kupunguza changamoto ya huduma hiyo.

Hata hivyo Mhe. Othman amesema kwamba Zanzibar kumejengeka utamaduni wakuwa wazuri wa kuanzisha miradi ya maendeleo lakini changamoto kubwa inabaki katika kuitunza na kuendeleza.

Hivyo amekumbusha mamlaka ya maji na viongozi wanaohusika kuhakikisha kwamba wanapanga na kuweka mikakati bora na sera imara za matumizi sahihi ya maji ili kupunguza tatizo la matumizi makubwa yasiyo ya lazima.

Amefahamisha kwamba ni muhimu katika kuifanya miradi kuwa endelevu kila mmoja miongoni mwa viongozi na wananchi kutimiza vyema wajibu wao ili wananchi wafaidi huduma zinatokanazo na fedha zao za kodi kwa miradi inayoanzishwa kuwa na  tija zaidi kwao na taifa kwa jumla.

Mhe. Othman amefahamisha kwamba Zanzibar kunahaja pia kwa viongozi katika ngazi zote ikiwemo halimashauri na wilaya na mikoa kuhakikisha kwamba wanakuwa na mwelekeo mpya katika mipango ya kutunza vianzio vya maji nchini ili visiendelee kuharibiwa.

Amesema kwamba eneo la magharibi ya Zanzibar ndio lenye vianzio muhimu  vya maji lakini sehemu kubwa ya maeneo hayo imekatwa miti na kujengwa nyumba jambo ambalo litaharibu sio tu mazingira na  kukumbwa na athari  za mabadiliko ya taibia nchi lakini pia na kukosa ama kuharibika vyanzo vya maji.

Amefahamisha kwamba serikali  imekuwa  ikiimarisha upatikanaji wa huduma  za maji mijini na vijijini kwa kuendeleza utekelezaji miradi ya maendeleo ikiwemo uchimbaji wa visima, ulazaji wa mabomba  sambamba na ujenzi wa matangi mapya ya kuhifadhia maji ili kuondoa changamoto hiyo kwa wananchi hivyo jujudi hizo lazima ziwe sambamba na utunzaji bora.

Aidha amesema kwa vile ofisi yake pamoja na mambo mengine lakini inajukumu lakusimamia mazingira hgivi itaanzisha maradi mkubwa wa kusaidia kuirejesha Zanzibar kuwa ya kijani ambao utahusisha wanajamii , viongozi wa halamashauri, wilaya na shehia  kwa kila mtu kupanda miti na kusaidia utunzaji wa mazingira.

Amesema paia kunahaja ya kujenga utamaduni wa kukirithisha kizazi upandaji wa miti ya aina mbali mbali katika kuhakimkisha utunzaji bora wa mazingira na kuhgifadhi vyema vyanzo vya upatikanaji wa maji nchini.

Mhe. Othman amesema kwamba serikali  inaishukuru sana ZAWA na Serikali ya India kupitia Benki yake ya EXIM sambamba na kuipongeza Kampuni ya Larsen and Toubro  Kampuni Elekezi ya M&S Crux ya Ushauri elekezi kwa kazi nzuri wanaoendelea kuifanya katika utekelezaji wa mradi huu.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa ZAWA Dk . Salha Mohammed Kasssim,  amesema kwamba mradi huo unatekelezwa kwa Mkopo kutoka EXIM Benk ya India kwa masharti nafuu ambao unajengwa kwa mashirikiano na wakandarasi watatu na utakapokamilika utakuwa umekamilisha skimu tatu za maji na jumla ya visima 64 vitachimbwa  kwa ajili ya kuondosha tatizo la maji Zanzibar.

Aidha amesema kwamba  kiasi cha shilingi  bilioni 2.5 zitatumiwa na serikali ili kugharamia ulipaji wa fidia za wananchi ambao mali zao zimeharibiwa kufuatia maeneo yao kupitiwa na mradi huo  ambao ni mkombozi kwa wazanzibari kwa kuwa utanufaisha idadi kubwa ya wananchi  katika shehia mbali mbali zikiwemo kianga , dole, mwembe mchomeke,Masingini , mtiufani pamoja na maeneo mengine jirani.

Mapema  Mgurugenzi wa mradi huo huo kutoka kampuni ya L&T kutoka nchini India amesema kwamba utekelezaji wa mradi huo unakwenda vizuri  na upo kwenye hatua kubwa  na kuiomba serikali na mamlaka zinazohusika kuharakikisha utoaji wa vifaa vinavyoingizwa katika utekelezaji wa mradi huo ili ukamilike kwa wakati.

 Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Maaji na Nishati Ndugu Joseoh Kilangi  amesema kwamba  uanzishwaji wa mradi huo ni sehemu muhimu katika utekelezaji wa miradi ya  uchumi wa mbluu ambayo haiwezi kutekelezeka vyema bila maji na umeme kuwa endelevu na kwamba lazima kuhakikisha kunakuwepomabadiliko katika kutimiza ndoto ya serikali ya kustawisha huduma kwa wananchi wake.

Mwisho

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Kupitia kitengo chake cha habari leo tarehe 08.01.2022.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.