Habari za Punde

Zanzibar kuanzisha mchezo wa Kabari

Katibu wa Baraza laTaifa la Michezo Zanzibar Said Kassim Marine akizungumza na Katibu wa Uganda Kabari Federetion Edgar Mujuni  kuhusu uanzishwaji wa Mchezo wa Kabari  Zanzibar huko Ofisini kwake Mwanakwerekwe Wilaya ya Magharib”B” Zanzibar.
Katibu wa Uganda Kabari Federetion Edgar Mujuni akitoa akipatia maelezo Katibu wa Baraza laTaifa la Michezo Zanzibar  Said Kassim Marine kuhusu uwanzishwaji wa mchezo huo Zanzibar wakati alipofika Ofisini kwake Mwanakwerekwe Wilaya ya Magharib “B” Mjini Zanzibar

Katibu wa Baraza La Taifa la Michezo Zanzibar Said Kassim Marine na Katibu wa Uganda Federetion Edgar Mujuni wakiwa katika picha ya paoja baada ya kuzungumza kuhusu kuanzishwa mchezo wa Kabari huko Mwanakwerekwe Miji Zanzibar.

Picha na Miza Othman BTMZ.


Na Miza Othman BTMZ 06/ 2/2023.

Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar limesema lipotayari kushirikiana na mchezo wa Kabari kwani kufanya hivyo kutapelekea kupiga hatua ya kuboresha sekta ya Michezo Zanzibar.

Hayo yameelezwa na Katibu wa Baraza hilo Said Kassim Marine wakati alipotembelewa na Katibu wa Uganda Kabari Federatin Edgar Mujuni huko Ofisini kwake Mwanakwerekwe Wilaya ya Magharib “B’” Unguja.

Alisema amemshukuru katibu Edgar Mujuni kwa kuamua makusudi kwa kuja kuendeleza mchezo huo kwani kufanya hivyo kutasaidia kuwainua vijana kujiajiri mchezo wa Kabari hapa Zanzibar.

Hata hivyo alisema baraza la Taifa la Michezo Zanzibar lipo tayari kusajili chama hicho na kutambulishwa kwa lengo la kujua nia na madhumuni ya mchezo wa Kabari  hapa Zanzibar.

Nae Katibu wa Uganda Kabari federetion  Edgar Mujuni alisema ameamua kuja Zanzibar  kuunga na Nchini  ya Uganda kupitia  mchezo wa Kabari kwa lengo la kuwaboresha Wachezaji wa mchezo huo na kufikia lengo walilokusudia.

Hata hivyo alisema  Mchezo huo utasaidia kuleta maendeleo Zanzibar na kuhakikisha matunda yanapatikana  kwa kuleta umoja na mashiirikiano ya upigaji hatua ndani ya  mchezo huo.

Aidha amelishukuru baraza hilo kwa kumpokea na kuweza kushirikiana na atahakikisha mchezo huo unaleta mafanikio kwani mchezo wa Kabari ni sawa na michezo mengine ikiwemo football na netboll.

Kwa upande wake Katibu wa Zanzibar Kabari Federetion Ahmada Abdalla Ahmada alisema wamefarajika kwa ujio wa katibu huyo watamuunga mkono na kuwa nae bega kwa bega ili kuhakikisha mafanikio ya mchezo huo yanapatikana.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.