Habari za Punde

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Amekutana na Tume ya Rais ya Kuboresha Taasisi za Haki Jinai

 

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akizungunza  mbele ya  Tume ya Rais ya kukusanya maoni ya Maboresho ya Taasisi za Haki Jinai  Tanzania , Jaji Mkuu mstaafu Mhe. Mohammed Chande Othman ( kulia kwa makamu)  na kushoto ni Makamu Mwenyekiti  wa Tume hiyo Ombeni Sefue.  Tume hiyo ilifika ofisini kwa makamu Migombani mjini Zanzibar kupokea maoni

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akimsikiliza Mwenyekiti wa Tume ya Rais ya kukusanya maoni ya Maboresho ya Taasisi za Haki Jinai  Tanzania , Jaji Mkuu mstaafu Mhe. Mohammed Chande Othman ( kulia kwa makamu)  na kushoto ni Katibu wa Tume hiyo Lauren Ndumbaro.  Tume hiyo ilifika ofisini kwa makamu Migombani mjini Zanzibar kupokea maoni

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema kuna haja ya Tanzania kuitumia fursa ya kuundwa Tume ya Rais ya Kuborosha Taasisi za Haki Jinai, nchini kupendekeza kuandaliwa mfumo bora utakaounda chombo rasmi na kuandaa sera bora itakayosimamia  vyema kimamlaka masuala yote ya Haki jinai Tanzania.

Mhe. Othman ameyasema hayo ofisini kwake Migombani mjini Zanzibar alipokutana na Wajumbe Tume hiyo iliyofika  ofisini kwa Makamu  kupokea maoni ya Mhe. Makamu kuhusiana na maboresho yanayohitajika katika taasisi za haki jinai na mfumo wa mahakama Tanzania.

Amefahamisha kwamba Tanzania kwa sasa inaonekana hakuna mfumo na sera rasmi za kusimamia taasisi za aina hiyo na kwamba ni jambo jema Tume hiyo kupendekeza kuundwa mfumo  rasmi na chombo kimoja chenye mamlaka kubwa pamoja na kuandaliwa sera itakayosimamia  masuala hayo kwa wepesi na kusaidia upatikanaji wa haki kwa jamii.

Mhe. Othman amesema kwamba hivi sasa utaratibu uliopo Tanzania ni mapungufu makubwa ambayo haina uwezo na haioneshi kuwepo utaratibu bora utakaosaidia watanzania kuendesha kwa wepesi taaisi na mfumo huo sambamba na kuzuia kujirejea rejea kwa makosa ya jinai ya aina mbali mbali yanayotendeka nchi.

Mhe. Makamu amesema maboresho mbali mbali yaliyofanyika katika mfumo wa sekta ya seheria nchi bado hayajakidhi haja na matarajio ya nchi kuwa na chombo kimoja  kinachosimamia masuala yote muhimu ya haki jinai kwani  yaliyofanyika yalizingatia zaidi urekebishaji wa kitaasisi kuliko mfumo unaohitajika sasa.

Mhe. Othman ameongeza kuwa Tanzania itakuwa imefanya jambo kubwa sana iwapo itatambua kwamba inahitajki kujenga upya mfumo  na utaratibu wake wa haki jinai ili kuondoa tatitizo la sasa lililopo.

Amefahamisha kwamba mfumo wa sasa pia unaruhusu makosa makubwa kutendwa na watu wenye nyadhifa, kubwa huku utaratibu na uwezo wa upelelezi wa polisi ukiwa dhaifu kutokana na kujengwa kisiasa kuliko kiuweledi zaidi, jambo ambalo athari inarudi katika kuzuia na kupeleleza makosa mbali mbali ya jinai na hivyo kulazimika kutumia maelekezo ya  viongozi wa siasa.

Mhe. Othman amesema mfumo huo wa polisi kupokea maelekezo ya kisasa inalifanya jeshi hilo kukosa na kujenga weledi  katika upelelezi wa makosa huku kazi hiyo ikiwa ni ya kitaalamu zaidi kuliko ya siasa.

Amesefahamisha kwamba kutokana na hali hiyo kunahaja ya kutathimini Idara za Upelelezi katika jeshi la Polisi kwamba iendelee kubakia ndani ya jeshi hilo ama iwe mamlaka mbali na jeshi la polisi linaloweza kufanya kazi zaidi ya kupeleleza kwa weledi mkubwa makosa tofauti ya jinai.

Mhe. Othman amefahamisha kwamba kwamba  hasa katika vipindi vya uchaguzi mfumo ulipo sasa wa polisi huendelea kupokea amri za wanasiasa na hivyo kuwafanya polisi kuendelea kutumika vibaya kinyume na malengo na matarajio ya jamii  ya watanzania jambo ambalo ni tatizo kuwepo hali hiyo.

Kuhusu Taasisi  na  Mamlaka kama za kuzuia rushwa , Tume ya Kuzuai na Kupambana na madawa ya kulevya  na mamlaka  nyengine za namna hiyo mhe. Othman amesema kwamba kwa mazingira ya Tanzania ni vyema  kuundwa kwa kuungwa pamoja chini ya chombo maalum kitakachokuwa na uwezo wa kitaalamu na rasilimali za kutosha za  kushuhulikia mambo maalum  ya namna hiyo chini ya maadili na kuweka wepesai zaidi kiutendaji.

Eneo jengine ambalo mhe. Othman alilizungumzia ni kuhusu masuala ya kitaalamu kama vile kwa Mkemia Mkuu, madaktari hali ilivyo sasa hawakutengenezwa kwenda kusaidia katika upatikanaji wa haki mahakamani lakini hutazama eneo la utaalamu zaidi katika viwango vyake vya Kitaasisi visivyomunganiko huku kukiwa hakuna mamlaka ya juu zaidi ya kusimamia zaidi.

Mapema mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Mstaafu Mohammed Chande Othman amesema kwamba tume hiyo inaendelea na kutekeleza jukumu lake la kukusanya maoni na taarifa kupitia wadau mbali mbali wakiwemo viongozi taasisi za haki jinai na wengineo kwa njia ya mikutano , madodoso  pamoja na maandishi ili kuwezesha kukusanya maoni na kuishauri serikali namna bora ya kuboresha mfumo wa haki jinai nchini Tanzania.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.