Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Atupele Mwakibete akizungumza wakati wa ziara yake katika Bandari ya Tanga kulia ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga Peter Milanzi
Na Oscar Assenga, TANGA.
MATUNDA ya uwekezaji katika Bandari ya Tanga yameanza kuonekana baada ya Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Atupele Mwakibete kueleza kwamba Bandari nhiyo imefanikiwa kukusanya mapato ya Sh.Bilioni 5 kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Machi mwaka huu.
“Hii ni kazi nzuri ya uwekezaji ambao umefanywa na Serikali hatua ambayo imeleta manufaa makubwa katika Bandari ya Tanga hivyo nitoe wito kwa wafanyabiashara kuitumia Bandari ya Tanga kutokana na kuwa na uweke"Alisema
Katika hatua nyengine,Naibu Waziri huyo alitoa muda wa mwezi mmoja kwa shirika la Reli Tanzani (TRC) kuhakikisha wanajenga miundombinu ya reli katika bandari ya Tanga ili kurahisha huduma za usafirishaji wa mizigo inayoshushwa kwenye bandari hiyo kuelekea maeneo mbali mbali ya nchi.
Awali akizungumza Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga Peter Milanzi alisema ndani ya kipindi Cha miezi mitatu wamepokea Meli kubwa tano ambazo zimebeba zaidi ya shehena ya mizigo Tani 130,000 .
Hata hivyo alisema kutokana na uingiaji wa Meli kubwa umesaidia kuwezesha ajira za muda mfupi 100 zimeweza kupatikana .
No comments:
Post a Comment