SERIKALI ya Mapinduzi ya
Zanzibar imesema ina azma ya kuendeleza na kufikia hatua kubwa zaidi kuifanya
sekta ya utalii kuendelea kuwa sekta mama ya uchumi wa Zanzibar kwa miaka
mitatu ijayo.
Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameyasema hayo kwenye mkutano wa wahariri na
waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari, Ikulu, Zanzibar ikiwa
ni kawaida yake ya kuzungumza nao kila mwisho wa mwezi.
Dk. Mwinyi alisema sekta ya Utalii Zanzibar, inachangia
asilimia 30 pekee ya pato la uchumi wa Zanzibar, ikilinganishwa na sekta
nyengine za Maendeleo, kupitia utalii wa Fukwe, Bahari na Mji mkongwe, ambao umeongeza
watalii wengi kiasi ya wawekezaji kuendelea kujenga hoteli nyingi kubwa pamoja
na nyumba za wageni za kisasa.
Aidha, Rais Dk. Mwinyi aliendelea kusisitiza umuhimu
wa Zanzibar kuwa na utalii wa kumbi za mikutano na kueleza kuwa ni chachu ya
kukuza uchumi wa nchi na kuongeza haraka fursa za biashara kwa Serikali, taasisi binasi na wananchi wa
kawaida, akitolea mfano wa mkutano mkubwa wa Chama cha Menejimenti ya Makatibu
Mahsusi (TAPSEA) na Chama cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka (TRAMPA) uliofanyika
Mei 27 mwaka huu maeneo ya Fumba, Zanzibar.
Rais Dk. Mwinyi alisema, kupitia mkutano huo,
Wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya bara na visiwani kutoka sekta za umma walikusanyika
pamoja kujadili masuala yao, hali iliyotoa fursa nyingi za uchumi na biashara
zikiwemo, nyumba za wageni kupokea wageni wengi, vyombo vya usafiri wakiwemo
bodaboda, taxi, na aina nyengine za usafiri, hoteli, wafanyabiashara wa
vyakula, matunda na wenyeji wa eneo lililowakutanisha washiriki wa mkutano huo
kwa namna moja ama nyengine walinufaika na fursa hizo.
“Ndio maana naendelea kuwasisitiza wananchi wa
Kilimani kuangalia kwa upana wa faida za utalii wa mikutano na fursa zake ili
wachangamkie fursa hizo zenye nia ya kuleta mabadiliko makubwa ya uchumi na
maendeleo” aliweka misisitizo Dk. Mwinyi.
Alisema, ikitoka sekta ya mafuta na gesi kuibuka na
kukua ghafla itachukua nafasi ya sekta ya utalii, kwani duniani kote mafuta na
gesi ndio seka kiongozi ya uchumi.
Akitoa ufafanuzi kuhusu ripoti ya Mkaguzi na
Mdhibiti Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG), aliyodaiwa kuiopokea kwa siri na
kutoitangaza kwa umma, Rais Dk. Mwinyi aliwatoa hofu wananchi na kueleza kwa
mujibu wa sheria lazima ripoti iwasilishwe mapema Baraza ya Wawakilishi na
bahati baraza lililkua limeanza hivyo, kulikuwa na haja ya kuwasilishwa mapema barazani
na baadae taratibu nyengine za kuitangaza zitafuata wiki ijayo.
“Wakati ripoti ya CAG inakuja kwangu, kuna utaratibu
wa kisheria kwamba Baraza la Wawakilishi likinza ndani ya wiki moja, siku saba,
lazima ripoti ya CAG iwe imeshapelekwa na kwa ratiba na safari tulizokuwa nazo
tukasema wacha tuipokee, tumkabidhi Waziri husika aiwasilishe Barazani ndani ya
kipindi hicho tusije tukavunja utaratibu wa kisheria” Alifafanua Dk. Mwinyi.
Alieleza ni kweli Baraza limeanza, ripoti ilipelekwa
na tayari imepangiwa siku ya kusomwa hadharani.
Akitolea ufafanuzi wa baadhi ya maswali aliyoulizwa
kwenye mkutano huo kuhusu ripoti ya CAG, yaliyowahusu baadhi ya wasaidizi wake
wakimwemo mawaziri na watendaji wengine wa Serikali endapo ripoti hiyo
itawakuta na ubadhirifu ndani ya Serikali anayoiongoza, Rais DK. Mwinyi
alieleza, kuna njia tatu za kuwachukulia kwanza ni hatua za kuitawala, ambapo Serikali
ikimgundua muhusika amehusika na uzembe fulani, kutoka kwenye ripoti ya CAG atatolewa
Serikalini.
Lakini pia Rais Dk. Mwinyi alieleza njia nyengine ya
jinai ambapo Serikali haihusiki sana, ikitokea mmoja wa wasaidizi wake
amekamatwa na ubadhirifu basi moja kwa moja atapelekwa mahakamani
nakueleza kwamba wapo baadhi yao wana kesi mahakamani kutokana na kukutwa na ubadhirifu
kwenye ripoti ya CAG kwa nyakati zilizopita.
Kuhusu changamoto za ubovu na uchakavu wa barabara
nyingi za mjini na vijini, Dk. Mwinyi alieleza Serikali imezamiria kuzifanyia
matengenezo makubwa barabara zote kwa kujibu wa viwango vya maeneo.
Alisema barabara za Mjini zitatofautiana na za
mashamba kwa viwango na uimara licha ya zote kutarajiwa kuwa kwenye uimara wa
hali ya juu lakini zitatofautiana kwa mujibu wa matumizi ya bara bara hizo
pamoja na madaraja na barabara za juu.
Nakueeleza kwamba barabara inayoelekea bandari
jumuishi ya Mangapwani itakua yakiwango cha hali ya juu zaidi kwa mujibu wa
matumizi yake ya shughuli za bandari.
Akizungumzia Ujenzi wa bandari Jumuishi ya
Mangapwani, Rais Dk. Mwinyi alieleza lengo la bandari hiyo ni kuhudumia kanda
nzima ya Afika Mashariki sio Zanzibar pekee.
Alieleza awali utaratibu wake ulianza mazungumzo na
watu wa Oman, kisha Serikali ilizungumza na watu kutoka Abu Dhabi, alieleza majadiliano
hayo yanafanywa baina ya timu ya serikali yenye nia ya kupata mkataba
utakaokuwa na maslahi ya nchi na bandari itakayojengwa kwa mujibu wa matakwa ya
Serikali ambayo lazima yazingatie sehemu za makontena, mafuta, nafaka, mafuta
na gesi eneo huru (Free zone na masuala ya kilojistiki)
Aidha, alieleza Serikali inatarajia kuyapandisha
hadhi, maeneo ya Mangapwani na Bumbwini kuwa miji mikubwa ya bandari.
Hata hivyo, Rais Dk. Mwinyi pia alitoa ufafanuzi
kufuatia safari yake ya kikazi mjini Doha, Qatar aliyoifanya hivi karibuni na
kuwaelezea waandishi wa habari kwenye mkutano huo alivyopata fursa kueleza
maeneo mbalimbali ya biashara na uwekezaji yanayopatikana Zanzibar na Tanzania
kwa ujumla.
IDARA YA MAWASILIANO,
IKULU ZANZIBAR
No comments:
Post a Comment